Toba

Toba ni zawadi ya kiroho inayotuwezesha kuunganisha nafsi zetu na Mungu wetu mwenye upendo. Ni njia ya kutuongoza katika kurekebisha mwelekeo wetu, kuachana na dhambi, na kuelekea nuru ya msamaha na neema ya Mungu. Tufatilie mafunzo mbalimbali yaliyotolewa katika Biblia kuhusu Toba.

Day 1 : Toba

Isaya 59 : 2

Dhambi zenu ndizo zzinazowatengs na Mungu wenu, dhambi zenu zinamfanya ajifiche mbali nanyi asiweze hata kuwasikia.

Maombi ni kupitia Zaburi ya 51.

Prayer Point

Baba naomba msamaha,nimekosa mimi, nimekosa sana mbele yako na hii dunia.Sitarudia  udhalimu, nirehemu katika ghadhabu yako kumbuka rehema. Nirudishie uso wako na fadhili zako.

Day 2 : Toba

Luka 13: 3

Nawaambieni hakika sivyo; lakini nanyi hali kadhalika, msipotubu mtaangamia kama wao.

Luke 13 : 2

No, I tell you; but nless you repent, you wil all likewise perish.

Maombi ni kupitia Zaburi ya 6

Prayer Point

Natubu bwana, nimekosa mimi nimekosa sana mbele yako ni hii dunia.Nirehemu ee Mungu. Usiniache niangamie kama wao.katikati ya ghadhabu yako kumbuka rehema. Nirehemu mja wako.

Day 3 : Toba

2 Mambo ya Nyakati 7 : 14

Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu; watajinyenyekeza na kuomba, na kunitafuta, na kuziacha njia zao mbaya; basi nitasikia toka mbinguni na kiwasamehe dhambi zao na kuponya nchi yao.

Maombi ni kupitia Zaburi ya 32.

Prayer Point

Baba najinyenyekeza mbele zako nikiomba toba na rehema.

Day 4 : Toba

Mnaposimama kusali, msameheni kila mtu aliyewakosea chochote, ili baba aliyembinguni awasamehe nyinyi makosa yenu.

Maombi ni kupitia Zaburi ya 38.

Prayer Point

Tafakari watu wote uliowabeba rohoni na kushindwa kuwasamehe lakini wasamehe wote na kuwaachilia rasmi.Hata kama walikukosea kiasi gani.Mpendwa usiposamehe unazuia rehema yako na Breakthrough.

Day 5 : Toba

Yeremia 3 : 22

Rudini, enyi watoto waasi, mimi nitaponya maasi yenu. Tazama, tumekuja kwako; kwa maana wewe u BWANA, Mungu wetu.

Maombi kupitia Zaburi ya 37

Prayer Point

Bwana tuponye na maasi yetu, tumekukimbilia wewe tusiaibke milele

Day 6 : Toba

Hosea 5 : 15

Nitakwenda zangu niparudia mahali pangu, hata watakapo ungama makosa yao na kuutafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.

Hosea 5 : 15

I will return again to My Place untill they acknowledge their offense.They will seek my face;in their affliction they will earnestky seek Me.

Maombi ni kupita Zaburi ya 102

Prayer Point

Baba nakubali uovu wangu nihurumie na kunionesha uso wako.

Day 7 : Toba

Yoeli 2 : 25 – 27

Nitawarudishia miaka ile iliyoliwa na nzige, kila kitu kilicholiwa na tunutu, papare na matumatu., hilo jeshi kubwa nililo waletea! mtapata chakula kingi na kutosheka; mtalisifu jina la mwenyezi Mungu, Mungu wenu aliye watendea mambo ya ajabu.Watu wangu kamwe hawata dharauliwa tena. Mtatambua kwamba mimi nimo miongomi mwenu, enyi Waisraeli; kwamba mimi Mwenyezi Mungu, ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine. Watu wangu kamwe hawatadharauliwa tena.

Prayer Point

Baba nimetubu toka moyoni. Pokea Toba yangu, unirehemu na kunifanyia urejesho kamili sawasawa na neno lako ulilolinena kupitia Nabii Yoel  kupitia Yoel 2 : 25 – 27

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Scroll to Top
× IT Help Desk