PART I : THE GOSPEL OF LUKE
Wapendwa tutasoma injili nzima ya luka, Mind you Luke is “the longest gospel of all” lakini tu “hii tutaifanya”, Wapendwa uvivu sio maisha! We will eat and leave no crumbs.
Tutasoma kama story ambayo ni first read na hii utafanya mwenyewe. Kama unasoma english version tumia “King James Version” hata english standardised version inafaa. Ukisoma kiswahili ndiyo kuna version kama zote, wewe jichagulie yoyote siyo kesi.
Tutasoma second version wote kwa mtiririko wa chapter by chapter na kuisummarise kila chjapter, We are talking 24 long chapters that Luke wrote!, He left no crumbs! and we the believers are going to read every word and may God help us!. After sucess of the long gospel of Luke, you will no longer be a pagan, as which Pagan read the gospel?, Absolutely None!.
Luka 1
1 Kwa kuwa watu wengi wamejitahidi kuandika habari za mambo yaliyotimizwa kati yetu,
2 kama vile walivyotufundisha wale waliokuwa mashahidi wa kwanza na watumishi wa neno,
3 nami nami nimeona vema, kwa kuwa nimefuatilia yote tangu mwanzo kwa bidii, kukuandikia kwa taratibu, ewe Theofilo mtukufu,
4 upate kujua hakika ya mambo yale uliyo fundishwa.
Kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji kunatangazwa
5 Zamani za Herode, mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, wa zamu ya Abiya, na mkewe alikuwa wa ukoo wa Haruni, jina lake Elisabeti.
6 Na wote wawili walikuwa wanyofu mbele za Mungu, wakienda katika amri zote na maagizo ya Bwana bila lawama.
7 Na walikuwa hawana mtoto, maana Elisabeti alikuwa tasa, na wote wawili walikuwa wamekwisha kuzeeka sana.
8 Basi ikawa, alipokuwa akifanya kazi ya ukuhani mbele za Mungu, kwa zamu ya kikundi chake,
9 kama desturi ya ukuhani ilivyokuwa, ilimpasa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana ili kufukiza uvumba.
10 Na mkutano wote wa watu walikuwa wakisali nje saa ya kufukiza.
11 Malaika wa Bwana akamtokea, amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia.
12 Zekaria alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, maana dua yako imeisikika, na mkeo Elisabeti atakuzalia mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
14 Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 Kwa maana atakuwa mkuu mbele za Bwana, hatakunywa divai wala kileo, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mama yake.
16 Naye atawaelekeza wengi wa wana wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
17 Naye atatangulia mbele zake katika roho na nguvu ya Eliya, kuwarejeza mioyo ya baba kwa watoto wao, na waasi waingie katika hekima ya wenye haki, ili kumtengenezea Bwana watu waliowekwa tayari.”
18 Zekaria akamwambia malaika, “Nitajuaje jambo hilo? Maana mimi ni mzee, na mke wangu ni mzee pia.”
19 Malaika akajibu akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu; nami nimetumwa niseme nawe, na kukuletea habari hizi njema.
20 Na tazama, utakuwa bubu usiweze kusema hata siku hayo yatakapotimia, kwa sababu hukuisadiki maneno yangu, yatakayotimia kwa wakati wake.”
21 Watu wakawa wakingoja Zekaria, wakastaajabu kwa kukawia kwake mle hekaluni.
22 Alipotoka hakuweza kusema nao, nao wakatambua ya kuwa ameona maono hekaluni; naye alikuwa akiwafanyia ishara, na kubaki bubu.
23 Ikawa, siku za utumishi wake zilipokwisha, alirudi nyumbani kwake.
24 Na baada ya siku hizo mkewe Elisabeti akachukua mimba, akajificha miezi mitano, akisema,
25 “Bwana amenitendea hivi siku hizo alizonikumbuka, ili aondoe aibu yangu mbele ya watu.”
Tangazo la Kuzaliwa kwa Yesu
26 Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu mpaka mji mmoja wa Galilaya, jina lake Nazareti,
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu jina lake Yosefu, wa nyumba ya Daudi; na jina la bikira huyo ni Mariamu.
28 Akaingia nyumbani kwake akasema, “Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.”
29 Naye alifadhaika sana kwa maneno hayo, akawaza moyoni salamu hiyo ina maana gani.
30 Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kwa Mungu.
31 Tazama, utachukua mimba, na kuzaa mwana, na jina lake utamwita Yesu.
32 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu; na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.
33 Naye atamiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.”
34 Mariamu akamwambia malaika, “Litakuwaje neno hilo, maana sijamjua mwanamume?”
35 Malaika akajibu akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.
36 Na tazama, jamaa yako Elisabeti, naye amechukua mimba ya mwana wa kiume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa.
37 Kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.”
38 Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema.” Malaika akaondoka akaenda zake.
Mariamu amtembelea Elisabeti
39 Mariamu akaondoka kwa haraka, akaenda hata mji wa milimani, mji wa Yuda;
40 akaingia nyumbani mwa Zekaria, akamsalimu Elisabeti.
41 Ikawa Elisabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto akacheza tumboni mwake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu,
42 akapaza sauti akasema, “Umebarikiwa wewe kuliko wanawake wote, na mzao wa tumbo lako umebarikiwa.
43 Nimepataje neema hii ya kwamba mama wa Bwana wangu anijie mimi?
44 Kwa maana tazama, sauti ya salamu yako ilipoingia masikioni mwangu, mtoto akacheza kwa furaha tumboni mwangu.
45 Na heri yake aliyoamini, kwa kuwa yatatimizwa yale aliyoambiwa na Bwana.”
Wimbo wa Mariamu (Magnificat)
46 Mariamu akasema,
“Roho yangu humwadhimisha Bwana,
47 na roho yangu imemfurahia Mungu Mwokozi wangu;
48 kwa kuwa ameutazama unyonge wa mjakazi wake.
Kwa maana tazama, tangu sasa vizazi vyote wataniita mbarikiwa;
49 kwa kuwa Mwenyezi amenitendea mambo makuu,
na jina lake ni takatifu.
50 Na rehema yake ni kwa wale wamchao,
kizazi hata kizazi.
51 Amefanya nguvu kwa mkono wake,
amewatawanya walio na kiburi
katika mawazo ya mioyo yao.
52 Amewaangusha wakuu kutoka viti vyao vya enzi,
akawainua wanyonge.
53 Wenye njaa amewashibisha mema,
na matajiri amewaondoa mikono mitupu.
54 Amemsaidia Israeli mtumishi wake,
kwa kumkumbuka rehema yake,
55 kama alivyowaambia baba zetu,
kwa Ibrahimu na uzao wake milele.”
56 Mariamu alikaa na Elisabeti kama miezi mitatu, akarudi nyumbani kwake.
Kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji
57 Basi, wakati wa kuzaa wa Elisabeti ulipotimia, alizaa mwana wa kiume.
58 Majirani zake na jamaa zake waliposikia ya kuwa Bwana ameiongezea rehema yake, walifurahi pamoja naye.
59 Ikawa siku ya nane walikuja kumtahiri mtoto, wakataka kumwita kwa jina la baba yake, Zekaria.
60 Mamaye akajibu akasema, “La! Bali ataitwa Yohana.”
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu katika jamaa yako aitwaye jina hilo.”
62 Wakamwashiria babaye, apendelee kuitwa jina gani.
63 Akaomba kibao, akaandika akisema, “Jina lake ni Yohana.” Wakastaajabu wote.
64 Mara kinywa chake kikafunguka, na ulimi wake ukaachiwa, akanena akimhimidi Mungu.
65 Hofu ikawa juu ya wote waliokaa karibu nao, na mambo hayo yote yakatajwa katika milima yote ya Uyahudi.
66 Wote waliosikia wakayaweka moyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
Unabii wa Zekaria
67 Baba yake Zekaria akajazwa Roho Mtakatifu, akatabiri akisema,
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli,
kwa kuwa amewajilia watu wake,
akawakomboa.
69 Naye ametuinulia pembe ya wokovu,
katika nyumba ya mtumishi wake Daudi,
70 kama alivyosema tangu mwanzo
kwa vinywa vya manabii wake watakatifu,
71 wokovu kutoka kwa adui zetu,
na mkononi mwa wote wanaotuchukia;
72 ili kuwatendea rehema baba zetu,
na kuukumbuka agano lake takatifu,
73 kiapo alichomwapia Ibrahimu baba yetu,
74 atuwezeshe sisi, tukiisha kuokolewa
na mikono ya adui zetu,
kumtumikia pasipo hofu,
75 katika utakatifu na haki mbele zake,
siku zetu zote.
76 Nawe, mtoto, utaitwa nabii wa Aliye juu,
kwa maana utatangulia mbele za uso wa Bwana
kumtengenezea njia zake,
77 kuwaambia watu wake habari ya wokovu,
katika kusamehewa dhambi zao,
78 kwa ajili ya rehema za Mungu wetu,
ambazo kwazo mchana kutuzukia kutoka juu,
79 kuwaangazia wakaao gizani na uvulini wa mauti,
kuielekeza miguu yetu katika njia ya amani.”
80 Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu rohoni; akakaa jangwani hata siku ile ya kujionyesha kwake kwa Israeli.
GENERAL SUMMARY
CHARACTERS:
- Zechariah – A jewish Priest from the tribe of Levi, described as a righteous man.
- Elizabeth – The wife of Zechariah also a levite, described as a righteous woman.
- John – Zechariah and Elizabeth’s newborn son.
- Mary – A young woman from the town of Nazareth.She was a virgin betrothed to be married.
- Joseph – Mary’s betrothed husband (similar to a fiance’).
- Gabriel – An angel who sent from the presence of God to bring good news.
Exploring Luke Chapter 1: The Dawn of Redemption
Where It All Begins
The events of Luke Chapter 1 unfold across key locations in Israel — Nazareth, a quiet village in Galilee; the hill country of Judea, rich with ancient history; and Jerusalem, the spiritual heart of the Jewish people. Each of these places sets the stage for one of the most profound introductions in the Bible: the coming of the Messiah and His forerunner.
Outline of Luke 1
1. Introduction (Luke 1:1–4)
Luke begins his Gospel with a statement of purpose. As a careful historian and follower of Christ, he explains that many have attempted to record the events of Jesus’ life, and now he is offering an accurate, orderly account — especially for Theophilus, so he may know the certainty of what he’s been taught.
2. John’s Birth Foretold (Luke 1:5–25)
In Jerusalem, during the time of King Herod, a faithful priest named Zechariah is serving in the Temple. While he carries out his sacred duties, the angel Gabriel appears to him with an extraordinary announcement:
-
He and his wife Elizabeth, though elderly and childless, will have a son.
-
This son, named John, will not just be a prophet — he will be the one who prepares the way for the Messiah.
-
He will be filled with the Holy Spirit even before birth and will turn many hearts back to God.
But Zechariah struggles to believe the message. In response, Gabriel strikes him mute until the prophecy is fulfilled — a divine sign of the certainty of God’s plan.
After his service in the Temple, Zechariah returns home, and just as the angel said, Elizabeth becomes pregnant. She recognizes this as God’s grace in removing her shame among people.
3. Jesus’ Birth Foretold (Luke 1:26–38)
Six months later, Gabriel is sent again — this time to a young virgin named Mary, living in Nazareth.
-
Mary is engaged to Joseph, a descendant of King David.
-
Gabriel tells her she will conceive a son through the Holy Spirit, and she is to name Him Jesus.
-
Her child will be called the Son of the Most High, and He will reign forever on David’s throne.
Although puzzled at how this will happen, Mary responds with faith and humility: “I am the Lord’s servant. May it be to me as you have said.”
Her willingness to accept God’s calling marks the beginning of a new chapter in salvation history.
4. Mary Visits Elizabeth (Luke 1:39–56)
Mary hurries to the hill country of Judea to visit Elizabeth. When she enters the house:
-
Elizabeth, filled with the Holy Spirit, blesses Mary and confirms everything Gabriel told her.
-
Even her unborn child — John — leaps in the womb at the presence of the unborn Jesus.
In response, Mary bursts into a beautiful song of praise, known as the Magnificat, celebrating God’s mercy, justice, and faithfulness across generations.
5. The Birth of John (Luke 1:57–80)
When Elizabeth gives birth, the entire community rejoices. On the eighth day, during the circumcision ceremony, everyone expects the baby to be named after his father, but Elizabeth insists: “He is to be called John.”
-
The people turn to Zechariah, who confirms the name in writing.
-
Instantly, his speech is restored — and he begins to praise God.
Zechariah then prophesies, speaking of God’s salvation, the role John will play in preparing the way, and the rising hope of the Messiah.
“And you, my child, will be called a prophet of the Most High;
for you will go on before the Lord to prepare the way for Him…” (Luke 1:76)
As the chapter closes, young John grows strong in spirit and lives in the wilderness until the time comes for his public ministry.
PART II: SPIRITUAL REVIEW
CHAPTER I
Naweza kusema palichangamka mapema, Chapter 1 tu mambo yalikuwa mengi lakini muda mchache.Mambo mazito ya kiroho yalitokea hapa ndani ya muda mfupi.
1.UJIO WA MALAIKA
Wapendwa huu ujio haukuwa mwepesi, Messenger of God alitua pande za Judea kwa kuhani zaka direct kutoka mbinguni na alikuja na ujumbe mzito.
He was very very direct and went straight to business, oyaa Zakaa! maombi yako yamesikiwa na mtapata mtoto na mkeo, na sio mtoto, Toto la kinabii, Litajazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni kwa mama yake.
Toto lita tangulia mbele zake katika roho ya Elia! The Elijah!!! Toto litawaokoa wengi sanaa na litafanya makubwa.
Kuhanizaka wa NOT SOOOOLD! Mmmhhhh! Not 1 beat! Aka weka karata zote mezani! Veve na mkewe wote age go home! Uzazi uplll? Huu huu wa menopause? 45 yrs hedhi inakoma kuashiria hakunaaa vai lililo baki bibi wewe! Kwisha habari yako. Zakaria hakutaka kuwa muongo! Aka limwagaaaa li doubt lake! “Atajuaje neno hili?”
And for some reasons it made Angel Gabriel furious! Beyond angry! Mpaka akajitambulisha: “Mimi malaika Gabriel, nae asimama mbele za Mungu mwenyewe! You dare question authenticity of my news????” Sasa tutaharibiana kazi!!! Kula chuma hiko cha ububu sababu hujui vya kuongea mpaka nikuoneshe hii kazi kwa vitendo.
Then malaika anabuka Galilaya kwa Bikira Maria. Yule yule Gabriel on the beat. Mary nae anapewa habari nzito za kubeba mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Ana jilipuaaaa! “Iwe kwangu kama ulivonena.”
What to take from this angelic encounter
1. Mungu hafungwi na biology wala science.
Bikira na tasa ambaye age go kweli kweli is scientifically and biologically impossible!. Bikira kuzaa, na wewe kwenda kazini hakiwezekani? Bikira kuzaa, na wewe kuolewa kipi kigumu zaidi? Tasa kikongwe kuzaa, na wewe kuvuka eneo la uchumi, kipi kigumu?
By the end of Luke Chapter 1: God 2 vs Science and Biology 0.
Malaika, na not only any malaika! Gabriel asimamae mbele za Mungu alikandamizaaaa: “Hakuna linaloshindikana mbele za Mungu.”
Mungu unayeshindwa kumuamini kwa mambo madogo sanaa yanayokunyima raha, ameshafanya mambo makubwaaa, mazitoooo na ya kustaajabishaaaa kama haya ya Bikira kuzaaaa mtoto wa kiume kinyume na sayansi na baiolojia. Wewe unashindwa kumuamini kwa vitu vidogo ambavyo vipo ndani ya mfumo???!!!!!
2. The Role of the Holy Spirit
Kuna protocal mbinguni, na japo Malaika alitanguliza taarifa, ila kazi ilifanywa na Roho Mtakatifu. Kazi nzito na ngumuuu zinafanywa na Roho Mtakatifu.
Pambana ubatizwe kwa Roho Mtakatifu lasivyo dunia ya impossible utaishia kuisoma kwenye Biblia kama hivi. Usharika na Roho Mtakatifu ni muhimu sanaa.
Maandiko yanapoishia, na akili za wanadamu ndipo Roho Mtakatifu anapoanziaaa. Kama unataka kuexperience the miraculous, role ya Holy Spirit haiwezi kuwa downplayed.
Kama Roho Mtakatifu aliweza kuwa juu ya Bikira na akabeba mimba, atashindwa kuwa juu ya interviews wakuchague wewe? Atashindwa kuwa juu ya wateja wanunue kwako? Atashindwa kuwa juu ya mpenzi wako akuchague wewe kukuoa?
Any deal ikiwa na usharika na Roho Mtakatifu is a DONE DEAL.
3. Mungu anaweza kutumia tatizo lako kujitukuza
Zakaria alikuwa kuhani, na sio kuhanitu! Maandiko yananyoosha: alikuwa kuhani aliyenyooka. Wote, na mkewe, walienda vile Mungu alivotaka. Walinyooka. Ila, for some reasons, hawakuwa na mtoto na age il go home.
Ndio maana Malaika alipomwambia Zakaria kwamba watazaa mtoto, ali-panic! Maana ni jambo alishaacha kulitegemea mdaaaa. Alishakubaliana na kukosa hiko kitu na kuendelea na maisha mengine.
Sasa Malaika kusema lile jambo, sio tu Mungu anaenda kulitimiza, bali litawapatia furaha sanaa. Kwake ilikuwa ghaflaaa sanaaa. Ilikuwa ngumu kumezaaa.
Yamkini hata wewe umekuwa disappointed eneo la kazi miaka na miaka! Wenzio wameenda kazini mpaka wanakaribia kustaafu. Yamkini umeingoja ndoa tangu binti kigori, sasa ni mwanamke wa makamo! Miaka 30 iliyo changamka—wanasema watoto wa mjini: 30 ya jioniii!
Mwambie Mungu, sawa sawa na andiko hili: bado unangoja ujumbe wako kutoka kwa Malaika kuhusu hili changamoto.
Sawasawa na hili andiko, unajua ipo siku Mungu atajitukuza kupitia wewe. Hajalishi kilomita zinasoma ngapi, na jua lishakuwa la jioni au usiku kabisaaa, una mngojea Bwana kama kuhani Zakaria. Kuliko kuhanizakaria—manake yule ilikuwa ghafla, wewe upo standby for God’s answers and grace! Anavyotaka Mungu, na wewe hivyo hivyo unataka.
Badooo unaamini Mungu atakufutia aibu kama alivyomfutia Elizabeth na Sarai.
Haya maandiko ndio ya wakulungwa ku-meditateeee huku unamtukuza Bwana kwa ukuu wake regardless unapitia nini. Usifocus kwenye ukubwa wa tatizo lako, rather ukuu wa Mungu. Zaka ali-yumba kidogo, aka-focus kwenye tatizo, akapigwa ububu. Don’t make the same blunder.
Tafakari kwa ukubwa wa show aliyoifanya Mungu hapa, Luke Chapter 1, na mwambie: Itimie kama ulivyotenda juu yangu pia Baba.
Luka Sura ya 2 (UV)
1. Kuzaliwa kwa Yesu
1 Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
2 Ilikuwa sensa ya kwanza iliyofanyika wakati Kirenio alikuwa mkuu wa mkoa wa Siria bible.com+15biblehub.com+15bible.com+15.
3 Basi wote waliokwenda walijiandikisha, kila mtu katika mji wake alikozaliwa.
4 Yosefu alitoka mji wa Nazareti akapanda hadi Bethlehemu, mji wa Daudi, kwani alikuwa wa ukoo wa Daudi.
5 Alifika akijiandikisha pamoja na mchumba wake Maria, ambaye alipokuwa mja mzito bible.com+4biblehub.com+4biblegateway.com+4.
6 Walipokuwepo huko, siku ya kujifungua ya Maria ikaje,
7 akamzaa mwana wake wa kwanza wa kiume, akamfunika vinguo na kumlaza horini kwa kuwa hawakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni youtube.com+15biblehub.com+15biblegateway.com+15.
2. Habari kwa Wachungaji
8 Usiku ule walikuwamo wachungaji wildani wakilinda kondoo zao.
9 Ghafla malaika wa Bwana akawatokea, na utukufu wa Bwana ukasang’azia pande zote – wakaogopa sana.
10 Malaika akawabaini: “Msiogope! Nimewaletea habari njema za furaha kuu, kwa watu wote.
11 Leo, katika mji wa Bethlehemu, amezaliwa Mwokozi – ndiye Kristo Bwana.
12 Hii ndiyo ishara: mtamkuta mtoto mchanga akiwa amefunikwa vinguo, amelazwa horini”
3. Maliku na Wasiwasi wa Mbingu
13 Mara akajitokeza wingi wa jeshi la mbingu, wakimshukuru Mungu na kusema: “Utukufu kwa Mungu huko mbinguni, na duniani amani kwa watu wanaompendeza”
14 Wachungaji wakasikia iliyoambiwa, wakae pamoja nao wakasikia, wakaenda haraka,
15 wakampata Mariamu, Yosefu, na mtoto amelala horini.
16 Walipomwona, wakasema iliwalete njia aliyoambiwa kuhusu mtoto huyo.
17 Wakati huo basi wote wakarudi wakiwa na furaha, wakamsifu na kumtukuza Mungu kwa yote waliosikia na kuona, kama ilivyoambiwa nao
4. Utokaji Hekaluni (Simeoni & Anna)
22 Baada ya kutimia kwa muda wa utakaso wa Musa, wakampeleka Yesu Yerusalemu kumtolea kwa Bwana,
23 kulingana na sheria iliyoandikwa: “Kila mtoto wa kiume wa kwanza atakabidhiwa kwa Bwana.”
24 Pamoja na sadaka – njiwa wawili au vifaranga wawili – kama agizo la Bwana
25 Huko Yerusalemu alikuwepo mzee mnyoofu na mcha Mungu, anayeitwa Simeoni,
26 Roho Mtakatifu alikuwa juu yake, na alijua huwa hangefa mpaka aangalie Kristo wa Bwana.
27 Ameongozwa na Roho hadi Hekaluni; walipoleta mtoto Yesu,
28 alimchukua mikononi mwake, akamshukuru Mungu na kusema:
29 “Sasa Bwana, niruhusu mtumishi wako aondoke kwa amani, kama ulivyoahidi,
30 kwa kuwa macho yangu yameona wokovu,
31 uliotayarishwa mbele ya mataifa, utukufu kwa watu wako Israel.”
32 Wazazi wake walistaajabu kwa maneno yaliyomzungumzwa juu ya yeye.
33 Simeoni akawabless, naye Maria na Yosefu wakayasikiliza maneno yote yasiyoyafahamu.
5. Nabii Anna
36 Kuna nabii mke, jina lake Anna, binti ya Penueli, ya ukoo wa Asheri.
37 Wakewa tangu ujana, sasa na mzazi na umri mkubwa, aliacha kuishi nyumbani, akitumikia Mungu kwa ibada, harakati na kufunga katika hekalu siku yote za maisha yake.
38 Huko karibu, alipoona mtoto huyo, alitamka shukrani kwa Mungu na kuzungumza juu ya Yesu kwa wale waliangeuka Yerusalemu
6. Yesu akakua na kukua Roho & Busara
39 Waliisha kukamilisha kila kinyume cha Sheria ya Bwana, walirudi Galilaya, jimboni Nazareti.
40 Mtoto akakua, akafundwa, akawa thabiti kwa nguvu, na hekima yake ikawa kubwa; neema ya Mungu ilikuwa juu yake
GENERAL REVIEW
CHARACTERS:
- Mary – A young woman from town of Nazareth, She was chosen by God to be the mother of Jesus the Messiah.
- Joseph – Mary’s betrothed husband (similar to a fiance’)
- Jesus – God’s Son and Mary’s child who was concieved mireculously by the Holy Spirit.
- Shepherds – Shepherds keeping sheep around Bethlehem who visited Jesus at his birth.
- Simeon- A righteous and devout man who Mary and Joseph meet in Jerusalem.
- Anna – A widow and phrophetess who served God in the Temple “with fasting and prayer night and day.”
WHERE:
-
The events of Luke Chapter 2 open in Bethlehem, the town where Jesus was born.
-
Nazareth, the hometown of Mary and Joseph, is briefly mentioned.
-
The remainder of the chapter takes place in Jerusalem, especially around the temple.
📜 OUTLINE:
✨ JESUS IS BORN (Luka 2:1–7):
-
Caesar Augustus decreed that the people of his empire should be “registered” (probably for tax purposes).
-
Joseph left Nazareth in Galilee and traveled to his hometown in Bethlehem for the registration.
-
Mary was close to giving birth when they departed.
-
When they arrived in Bethlehem, Mary gave birth.
-
There was no room in the inn, so they laid their son in a manger.
🐑 THE SHEPHERDS VISIT NEWBORN JESUS (Luka 2:8–21):
-
Following the birth of the child, an angel appeared to shepherds in the fields around Bethlehem.
-
The angel told them the newborn baby was the Savior and Christ the Lord.
-
They were told they would find Him in a manger and wrapped in swaddling cloths.
-
Suddenly a multitude of heavenly beings were visible to the shepherds and they heard them praising God.
-
The shepherds went and found the child in the manger and told Joseph and Mary what they had seen.
-
Eight days after his birth, the baby was circumcised and named Jesus according to the angel’s instruction.
🏛 JESUS, MARY, AND JOSEPH VISIT JERUSALEM TO KEEP THE LAW OF MOSES (Luka 2:22–38):
-
In order to keep some of the Old Testament commands regarding childbirth, Jesus’ family visited Jerusalem.
-
This took place approximately 1 month after Jesus’ birth.
-
They took an offering of either two turtledoves or two young pigeons according to God’s law in Leviticus 12:6–8.
-
In Jerusalem, they met a man named Simeon whom God had promised would see the Messiah before he died.
-
Simeon took Jesus in his arms and worshipped God for allowing him to see the future Savior.
-
In the Temple, Mary and Joseph met a prophetess named Anna.
-
When she saw Jesus she also worshipped God and started telling everyone about Him.
-
Following these events, Joseph, Mary, and Jesus returned to their home in Nazareth.
🔍 JESUS’ PARENTS LOSE HIM IN JERUSALEM (Luka 2:41–52):
-
12 years later, Jesus and His parents returned to Jerusalem to celebrate the Passover Feast.
-
When returning home, Jesus’ parents assumed He was with their relatives and traveling companions.
-
After a day’s journey, they realized Jesus wasn’t with them and returned to Jerusalem.
-
They searched for 3 days before finding Him in the Temple talking to the religious teachers.
-
When He was located, He asked His parents,
“Did you not know that I must be in my Father’s house?”
PART III: SPIRITUAL REVIEW
CHAPTER 2
Wapendwa Chapter 2 is all about the humble beginnings of Jesus Christ, Contrary na mategemeo na mapokeo ya Wayahudi wengi ambao walitegemea Yesu atazaliwa kwenye familia ya kifalme, like ukoo wa Herode maybe au Kayafa basi hata kwa kuhani. Yaani atakuwa na watu wazito nyuma yake, Atakuwa na supreme powers nyuma yake za dunia hii. Nepo Baby flani, Toto flani la kushua lina zaliwa na machawa wapo standby ku bobisha bobisha pale, tarambee kama zote.
Wapendwa sawa Yesu ni uzao wa mfalme wa Daudi ila siyo Daudi ile ya zama zile za mfalme tajirii suleiman lenye fahari zake, sio mwana wa Daudi washed out selemala Yosefu. Maisha yake magumu hatari, yaani anakosa hata chumba hotelini, anatandika kwenye zizi kweli??, Hata ukisoma injili ya Mathayo utaona Herode ana ambiwa kuna mfalme kazaliwa zizini and he was like, What in the hell??, Mfalme gani anazaliwa zizini?, Last time I checkedmimi ndiye mfalme wa Mayahudi, zizi na mfalme vinakaaje kwenye sentensi moja.
KUZALIWA KWA YESU: UJUMBE WA NEEMA, UNYENYEKEVU NA NGUVU YA MUNGU
Mungu alikuwa na kusudi lake maalum Yesu kuzaliwa katika hali ya unyenyekevu. Haikuwa makosa kwamba alizaliwa zizini, kwenye familia ya kawaida kabisa. Hili lilikuwa ni fundisho kubwa kwa kizazi chote.
Mwisho wa yote, Yesu alifahamika kama Mfalme — lakini hakuwa na ufalme wa kidunia wala majeshi. Alikuwa “jeshi la mtu mmoja!” Alijulikana kama mwalimu, lakini hakuwahi kuwa na shule. Alijulikana kama mponyaji, lakini hakusomea udaktari. Na tusisahau kwamba alizaliwa zizini, kwa baba seremala na mama housewife.
Maandiko yako wazi juu ya hili. Hakuna mambo ya fumbafumba au “window dressing” kwenye maandiko. Mambo yamewekwa peupe!
1. Humble Beginnings ya Yesu: Ujumbe kwa Waja wa Mungu
Unapochunguza hali aliyoanzia nayo Yesu, unagundua ujumbe mkubwa:
Unaweza kuanza na hakuna na kuwa mmoja wa wakubwa kabisa.
Ukiangalia “starter pack” ya Yesu, unaweza kukata tamaa kwa maoni ya kibinadamu. Biblia inasema:
“Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.” (Luka 2:40)
Ndiyo hiyo tu aliyopata kutoka kwa Baba yake wa mbinguni — neema ya Mungu!
Lakini sisi leo hatuoni kama neema inatosha. Tunataka pia:
- Destiny helpers
- Wachungaji wa nguvu
- Maeneo mazuri ya huduma
- Bajeti za matangazo ya redio
- Mavazi ya kifahari ya huduma
- Magari ya bei mbaya ya kuonyesha “aura ya kifalme”
Lakini Yesu alipewa neema tu — na akaikamilisha kazi ya wokovu. “The finished work of Christ” haikuhitaji bajeti ya mabilioni. Ilihitaji tu neema na utiifu.
2. Mungu Ana Jitukuza Mwenyewe
Mungu hahitaji msaada wa wanadamu dhaifu ili kutukuzwa. Ungetegemea Yesu apokelewe na wakuu wa dunia — Herode, Kaisari, Pilato — lakini la! Malaika waliwatuma wachungaji wa Betlehemu, watu wa kawaida waliokuwa hata hawajasoma, kunukia mbolea!
Mungu alituma ujumbe: Anaweza kutumia yeyote kwa kazi yake.
Usipokuwa makini, unaweza kupishana na msaada wa Mungu kwa sababu haufanani na matarajio yako ya kifahari. Destiny helpers wako wanaweza kuja wakiwa wamechoka na kuvaa kawaida — lakini ndani yao mna msaada wako wa mbinguni!
Hata Mariamu alipata ujumbe wa ujauzito kutoka kwa Gabrieli — malaika anayeishi mbele za Mungu. Hakufikiri kupinga, alitii, akazaliwa mtoto wa wokovu.
3. Yesu Alizaliwa Kutukomboa Sisi
Kama bado huamini, basi kaa bila wokovu — lakini si kwa sababu hujaambiwa!
Katika Luka 2, jambo hili lilisemwa na:
- Malaika (Luka 2:10-14)
- Simeoni, mzee mwenye haki (Luka 2:25-35)
- Nabii Ana, mjane mzee aliyekaa hekaluni (Luka 2:36-38)
Wote walithibitisha: Yesu alizaliwa ili atuokoe.
Kwa hiyo, kama umekuwa ukisikia tu kuhusu Yesu, leo umemsoma. Unaanza kumjua uzuri wake, neema yake, na wokovu wake.
4. “Imenipasa Kuwamo Katika Nyumba ya Baba Yangu”
Yesu alipokuwa na miaka 12 alisema:
“Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?” (Luka 2:49)
Yesu alipenda hekalu tangu utotoni. Alikaa huko, alisikiliza, aliuliza maswali — kwa unyenyekevu. Japo alikuwa Mwana wa Mungu, hakujionyesha wala kujigamba.
Yesu alianza kujifunza akiwa na miaka 12, hadi alipoanza huduma akiwa na miaka 30. Hiyo ni miaka 18 ya kujifunza kwa kina — na huduma yenyewe aliifanya kwa miaka 3 tu, lakini akaihitimisha kikamilifu!
Leo, wengi hawataki kukaa nyumbani kwa Baba, hawataki kujifunza. Wanataka kuanza huduma leo na kesho iwe ya kimataifa. Wanaomba maono ya Musa na sauti za malaika, lakini hawapo tayari kujifunza kwa unyenyekevu.
Yatupasa sote kukaa nyumbani kwa Baba ili tufikie viwango alivyotuwekea.
Ikiwa hujui kukaa, Mungu hatakuja kukuchota porini — jifunike, tulia, jifunze. Njia za Mungu si njia zako.
Luka 3 – Yohana Mbatizaji Aandaa Njia
1. Yohana Aanza Kuhubiri
1 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alipokuwa gavana wa Yudea, Herode akiwa mtawala wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mtawala wa Iturea na Trakoniti, na Lisania mtawala wa Abilene,
2 wakati ambao Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu, neno la Mungu lilimjia Yohana, mwana wa Zakaria, akiwa jangwani.
3 Basi Yohana alikwenda katika sehemu zote za kandokando ya mto Yordani, akihubiri kwamba watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
4 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya:
“Sauti ya mtu aliaye jangwani:
‘Itayarisheni njia ya Bwana,
nyoosheni mapito yake.
5 Kila bonde litajazwa,
kila mlima na kilima vitashushwa;
palipopinda patanyooshwa,
njia mbaya zitafanywa kuwa laini.
6 Na watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
2. Onyo kwa Mafarisayo na Wengine
7 Yohana aliwaambia watu wengi waliomwendea wapate kubatizwa:
“Enyi wazao wa nyoka! Nani aliyewaonya mkimbie ghadhabu inayokuja?
8 Zaaeni matunda yanayoonyesha kuwa mmetubu kweli. Wala msianze kusema mioyoni mwenu, ‘Sisi ni watoto wa Abrahamu.’ Nawaambieni, Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka katika mawe haya.
9 Hivi sasa shoka limekwisha wekwa karibu na mzizi wa miti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.”
3. Maisha Mapya ya Watubu
10 Watu wakamwuliza, “Basi tufanye nini?”
11 Akawajibu, “Aliye na mashati mawili na amgawie asiye na hata moja; aliye na chakula afanye vivyo hivyo.”
12 Wakaja pia watoza ushuru wapate kubatizwa, wakamwuliza, “Mwalimu, tufanye nini?”
13 Akawaambia, “Msitoze kodi zaidi ya ile mliyoamriwa.”
14 Wakamwuliza pia askari, “Na sisi tufanye nini?” Akawaambia, “Msinyanyase mtu wala kumshtaki kwa uongo; ridhikeni na mshahara wenu.”
4. Yohana Aelekeza kwa Yesu
15 Watu walikuwa wakingojea kwa hamu na wote walikuwa wakijiuliza mioyoni mwao kama Yohana ndiye Kristo.
16 Yohana akawajibu wote, “Mimi nawabatiza kwa maji; lakini anakuja mwenye uwezo kunizidi mimi, ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 Mikononi mwake ana chombo cha kupuria nafaka, ataipura nafaka yake, atakusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
18 Kwa maonyo mengine mengi aliwahubiria watu habari njema.
5. Yohana Afungwa
19 Lakini Herode mtawala, ambaye Yohana alimkemea kwa kumchukua Herodia, mke wa ndugu yake, pamoja na uovu mwingine aliokuwa akitenda,
20 akaongeza uovu huu kwa kumfunga Yohana gerezani.
Ubatizo wa Yesu
21 Watu wote walipokuwa wakibatizwa, Yesu naye alibatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka,
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama hua, na sauti ikasikika kutoka mbinguni:
“Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
Nasaba ya Yesu Kristo
23 Yesu alipokuwa na miaka karibu thelathini, alianza huduma yake. Alijulikana kuwa mwana wa Yosefu, mwana wa Eli,
24 mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
25 mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
26 mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shimei, mwana wa Yoseki, mwana wa Yoda,
27 mwana wa Yohana, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 mwana wa Yosua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
30 mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
31 mwana wa Melea, mwana wa Mainani, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 mwana wa Aminadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
34 mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
37 mwana wa Methusela, mwana wa Enoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
38 mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.
PART IV: SPIRITUAL REVIEW
CHAPTER 3
Wapendwa neno la Mungu linamfikia Yohana mwana wa Zakaria jangwani akahubiri ubatizo wa toba uletao ondoleo la dhambi. Sauti ya mtu aliye nyikani ilisikika na unlike Jesus, John the baptist was always direct!, Never used parables, alichokisema ndicho alicho maanisha, na alichokimaanisha ndicho alichokisema.
Nyoosheni mapito yenu, sawazisheni mabonde kwenye maisha yenu. Yohana mbatizaji hakuwa na mbambamba kwenye kukemea dhambi na hiki ndicho kilikuja kumgharimu maisha yake.
Ikatokea aka mkaripia Herode juu ya mke wa kaka yake ambaye Herode kulikua na namna za ujanja.
Herode alimuweka jela Yohana Mbatizaji! Sasa, kuna siku Herode alikuwa na karamu la kukata na shoka! Binti yake akacheza vizuri sana mbele za wageni. Herode akajichanganya, akamuahidi aombe chochote atampa.
Binti akamuuliza mama yake, “Niombe nini?” Mama yake akamwambia, “Omba kichwa cha Yohana!” Binti akaomba. Na sababu mfalme alishajicommit kumpa chochote atakachoomba, ikala kwa Yohana Mbatizaji.
Prior Herode hajamuweka Yohana gerezani, Yohana Mbatizaji used to teach and baptize! Na among many, Yesu was also baptized with John the Baptist.
Ubatizo wa Yesu Ulikuwa Tofauti
Ubatizo wa Yesu ulikuwa tofauti na wengine woteee! Yesu akiwa anabatizwa, sauti ilitoka juu mbinguni kumu-endorse Yesu.
Luka 3:21
Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka;
Luka 3:22
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni,
“Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.”
Cha kuzingatia:
Yesu hakuanza kazi rasmi kabla ya kubatizwa kwa maji na Yohana, na kushukiwa na Roho Mtakatifu baada ya ubatizo.
Prior ubatizo huu wa Yesu, ukisoma Injili zingine Yesu alishapiga muujiza wa Cana – lakini ilikuwa bado haijawa official kwenye “live” na miujiza vile inavyotakiwa!
Watu Wengi Mnataka Kufanya Mambo Vice Versa!
Mnataka kufanya the miraculous kabla ya kubatizwa kwa Roho Mtakatifu – ndo maana mnakwama BIG TIME.
Mnakuwa mpo nje ya protocol na mfumo.
Before God anounces you publicly (iwe kazini au kwenye biashara au mahusiano), lazima kwanza ahakikishe umebatizwa kwa Roho Mtakatifu ili kuwe na mawasiliano baina yenu! Uweze ku-discern maelekezo yake.
Wengi Mnakosa Discipline na Consistency
Wengi mnakosa discipline na consistency ya kuweza kubatizwa katika Roho na kweli! Lakini hapo hapo mnatumia nguvu kubwa kumfosi Mungu awa-announce to the world!
👉 It will NEVER work!
👉 It is a LIE.
Mungu akiku-announce bila kubatizwa na Roho Mtakatifu, it is a recipe for disaster. Ni suala la muda.
Mtu, watu wataona hun majibu! Watu watakuja kwako wanataka majibuuu na wewe majibuuu hunaaaa!
Hujadhalilika mpaka hapo?
Public Announcement Without Spiritual Equipping = Aibu
Mungu akiku-announce kwamba yupo na wewe, upewe Head wa Sales! Kama umebatizwa kwa Roho Mtakatifu – haina shida. Atakupa:
-
Strategy za kupata wateja
-
Kibali cha kuridhika wateja
Kama hujabatizwa kwa Roho Mtakatifu, utaimba “Hallelujah!”
👉 Mana yake maboss wanataka MAJIBU!
Everybody wants answers from you – and you have NONE to give!
Huna mawasiliano na Roho Mtakatifu.
Matokeo yake sasa unaanza kutunga vitu.
Unaweweseka kama unaoga nje.
Roho Mtakatifu = Maisha ya Ushindi
Baada ya kubatizwa Yesu – ndo Roho Mtakatifu akamshukia.
Na baada ya hapo, ilikuwa SHOW TIMEEEEE!
Funga kazi! 🔥🔥🔥
Ni miujiza back to back mpaka siku anasulubiwa!
Madhehebu Mengi Yanadownplay Ubatizo wa Roho Mtakatifu
Madhehebu mengi yana-downplay ubatizo wa Roho Mtakatifu!
But listen to this:
HOLY SPIRIT IS THE FUTURE OF RELIGION!
Maana anakupa strategy LIVE LIVE!
Bora ukahaha hahaaaa hata miaka 5 unausaka ubatizo wa Roho Mtakatifu.
👉 Siku ukiupata kazi umeimalizaaaa! 😤💥
🕊️ Ubatizo wa Roho Mtakatifu sio luxury – ni mahitaji ya msingi ya safari ya kiroho na maisha ya ushindi.
Usikubali kuitwa hadharani kabla hujapakwa mafuta!
Luka 4
1 Yesu, akijaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho mpaka nyikani,
2 akiwa amejaribiwa na Ibilisi siku arobaini; wala hakula kitu katika siku hizo; hata zilipotimia, aliona njaa.
3 Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate.
4 Yesu akamjibu, Imeandikwa ya kwamba Mtu hataishi kwa mkate tu.
5 Kisha Ibilisi akampandisha juu, akamwonyesha falme zote za ulimwengu kwa dakika moja.
6 Ibilisi akamwambia, Nitakupa mamlaka haya yote, na fahari yake; kwa sababu nimekabidhiwa mimi, nami humpa mtu nitakaye.
7 Basi wewe ukisujudu mbele yangu, yote yatakuwa yako.
8 Yesu akajibu, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.
9 Akamleta Yerusalemu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa;
10 kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake wakulinde;
11 na mikononi mwao watakuchukua, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
12 Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
13 Ibilisi alipokwisha kumaliza majaribu yote, alimwacha hata wakati unaofaa.
14 Yesu akarudi Galilaya kwa nguvu ya Roho, habari zake zikaenea katika nchi zote zinazozunguka.
15 Akaanza kufundisha katika masinagogi yao, akaheshimiwa na watu wote.
16 Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; akaingia katika sinagogi siku ya Sabato kama ilivyokuwa desturi yake, akasimama ili asome.
17 Akapewa kitabu cha nabii Isaya. Alipokifungua akakuta mahali palipoandikwa:
18 Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa maana amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema;
amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona,
kuwaweka huru waliopondeka,
19 na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.
20 Akapetisha kitabu, akamrudishia mtumishi, akaketi; macho ya wote waliokuwamo katika sinagogi yakamkazia.
21 Akaanza kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia masikioni mwenu.
22 Wote wakamshuhudia, wakastaajabu maneno ya neema yaliyotoka kinywani mwake, wakasema, Huyu si mwana wa Yusufu?
23 Akaambia, Hakika mtaniambia mithali hii, Tabibu jiponye nafsi yako; mambo tuliyosikia kuwa ulitenda Kapernaumu, yafanye na hapa kwao.
24 Akasema, Amin nawaambia, Hakuna nabii anayekubaliwa kwao.
25 Lakini nawaambia kweli, Palikuwa na wajane wengi katika Israeli siku za Eliya, mbingu zilipofungwa muda wa miaka mitatu na miezi sita, njaa kuu ikawa juu ya nchi yote;
26 lakini Eliya hakutumwa kwa mmoja wao, ila kwa mwanamke mjane kule Sarepta ya Sidoni.
27 Na palikuwa na wenye ukoma wengi katika Israeli zamani za nabii Elisha; wala hakuna hata mmoja aliyesafishwa, ila Naamani Mshami.
28 Wote waliokuwamo katika sinagogi waliposikia haya, wakajaa ghadhabu,
29 wakaondoka, wakamtoa nje ya mji, wakampeleka hata kilele cha mlima ambao mji wao umejengwa juu yake, ili wamtupie huko chini.
30 Lakini yeye akapita katikati yao, akaenda zake.
31 Akaenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, akawa akiwafundisha siku za Sabato.
32 Wakashangaa mno kwa mafundisho yake, kwa sababu neno lake lilikuwa na mamlaka.
33 Palikuwamo katika sinagogi mtu mwenye pepo mchafu, mwenye roho ya pepo mbaya; akalia kwa sauti kuu,
34 Akisema, Ah! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Nakujua u nani, Mtakatifu wa Mungu.
35 Yesu akamkemea, akisema, Nyamaza, mtoke. Pepo akamtupa katikati, akamtoka, bila kumdhuru hata kidogo.
36 Wote wakastaajabu, wakasema wao kwa wao, Ni neno gani hili? Kwa maana kwa mamlaka na uweza huwaamuru pepo wachafu, nao hutoka.
37 Habari zake zikaenea kila mahali katika nchi ile yote.
38 Akatoka katika sinagogi, akaingia nyumbani kwa Simoni. Mama mkwe wa Simoni alikuwa na homa kubwa, wakamwomba kwa ajili yake.
39 Akasimama karibu naye, akakemea ile homa, ikaacha. Mara akainuka, akawaendea huduma.
40 Jua lilipokuwa likitua, wote waliokuwa na wagonjwa wa maradhi mbalimbali wakawaleta kwake, akaweka mikono juu ya kila mmoja wao, akawaponya.
41 Pepo pia waliwatoka wengi, wakipiga kelele, wakisema, Wewe ndiwe Mwana wa Mungu. Lakini aliwakemea, asiwaruhusu kunena; kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.
42 Kulipopambazuka akaondoka, akaenda mahali pasipokuwa na watu. Makutano wakamtafuta, wakamfikia, wakataka kumzuia asiende zake.
43 Akawaambia, Imenipasa kuihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana kwa ajili hiyo nalitumwa.
44 Akaenda akihubiri katika masinagogi ya Uyahudi.
SPIRITUAL REVIEW
CHAPTER 4
Yesu anakataliwa kwao Nazareth na dakika za mwanzoni kabisa wa huduma yake anawahakikishia hawajapata kitu toka kwake, hatotenda muujiza hata mmoja. Mpendwa ukiangalia juu unaweza sema mbona kama Yesu alijiwahi kuwa defensive and judgemental against the Nazarethians?!!!, ukipekenyua why?, Utaona they surely deserve what they got.
Wapendwa Yesu alichokisemani ukweli mtupu, he spoke only truth and nothing but absolute truth, Roho wa Bwana alikuwa juu yake kweli?, Absolutely! chapter 2 alijazwa roho mtakatifu.
Luka 4: 18
Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema.Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, kuwaacha huru walioteswa.
Yesu alikuwa mpyaaaa kabisa kwenye huduma! Fresh from Jordan, just anointed, akapitia wilderness, kashinda majaribu. Sasa hapa Luka 4, ni mwanzo wa huduma yake hadharani. Na wapi kaamua aanze? Nazareti! Kwao kabisa!
Yaani, kama ni “charity begins at home”—Yesu alithibitisha hilo.
Anaingia sinagogi kama kawaida yake. Anapewa chuo cha nabii Isaya. Anafungua, anasoma:
“Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa maana amenitia mafuta… kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.”
(Luka 4:18-19)
Akamaliza kusoma, akaketi. Akasema:
“Leo andiko hili limetimia masikioni mwenu.”
(Luka 4:21)
🔥 Na hapo ndipo watu wa Nazareti wakaanza kupata pressure ya kiroho! Walianza kuhoji, “Huyu si mwana wa Yusufu huyu?” Ubabaifu ukaanza. Yaani walimsikia amefanya makubwa kule Kapernaumu na kwingine, lakini kwao hawataki hata aongee.
They just didn’t believe Him!
UBABAAIFU NI WA VIZAZI
Yesu hakustushwa! Hakushangaa! Akawachana live:
“Amini nawaambia, hakuna nabii anayekubalika kwao.”
(Luka 4:24)
Ubabaifu wao haukuwa ishu kwake. Aliwaambia wazi kabisa, veve sio wa kwanza kukataliwa kwa kwao. Wala sio wa mwisho. Ubabaifu ni hereditary dysfunction — product ya vizazi na vizazi.
Hakuwa na stress, hakuwalilia, hakufa kwa sononeko.
🔥 HANDLE REJECTION LIKE JESUS 🔥
Yesu alikataliwa Nazareti. Walitaka hata kumsukuma bondeni afe.
But guess what?
“Akapita kati kati yao, akaenda zake.”
(Luka 4:30)
Waliotaka kumtupa bondeni—walibaki wamepigwa butwaa.
Hili ni somo kwa kila mtu anayeumizwa na rejection.
You too—PITA KATI KATI YAO!
Wanaokukataa hawamalizi hatima yako. Hawawezi kufuta mwaka wa Bwana ulio amriwa juu yako!
🔁 MAHUSIANO YANAKUKATAA?
Mwanaume umempenda balaa, lakini hajakupenda.
So what? Dunia ina wanaume billion 7!
Kama huyo hakutaki, pita katikati yake, songa mbele!
Tangaza mwaka wa Bwana ulio amriwa kwenye ndoa yako.
Wewe ni nabii juu ya maisha yako.
🧳 KAZI IMEKUKATAA?
Umekataliwa kazini? Umefukuzwa?
So what? Kazi ni nyingi. Fursa zipo.
Usikubali stress za kufukuzwa zikufanye kuwa mlevi mbwa au malaya mchafu!
Hiyo ndio raha yao—kukuharibu.
DON’T GIVE THEM THAT SATISFACTION.
Tafuta kazi nyingine. PITA KATI KATI YAO.
💼 BIASHARA YAKO IMEKUFA?
Kuna mtu alikuuliza, “Biashara yako ikifa itakuwaje?”
Jibu lako linapaswa kuwa:
“Haitakuwa kitu! Nitafungua nyingine!”
Zishakufa nyingi kabla yake, bado upo.
Na bado unatamba nazo.
💍 HAKUTAKI KUOA?
Mwanaume amekataa kukuoa?
PITA KATI KATI YAKE.
Tangaza mwaka wa Bwana ulio amriwa juu ya ndoa yako.
Funga ndoa na mtu anayeona dhamani yako.
Usilalamike. Wengine wanakataliwa hata wakiwa na watoto 3,
tumbo linafunika kipapa, nyonyo ziko tumboni,
michirizi kama ramani ya kuzimu…
Hata vioo vinaogopa kukuangalia!
Still—wana watu.
Mtu anayeweza kukustiri anakwambia kafie mbele,
anachukua kitoto cha 2000!
PITA KATI KATI YA HALI HIYO.
🌪️ UZEE UNAANZIA ROHONI
Hata upake anti-aging, collagen kopo tatu kwa wiki,
ukishazeeka rohoni—imekula kwako.
Uzee huanza rohoni, si kwenye ngozi.
Ukibaki kulia why me? why now? hautaona mlango wa Mungu.
Learn from the Master himself — God Incarnate.
Yesu aliwaambia wazi, “Andiko limetimia masikioni mwenu.”
Wakapaniki! Wakauliza, “Roho gani iko juu yako? Hiyo mafuta gani? Huyo ni nani?”
📖 MAANDIKO HAYABADILISHWI NA UBABAAIFU
Yesu hakutunga neno jipya.
Alisoma kile kilichoandikwa na nabii Isaya, akasema:
“Leo andiko hili limetimia.”
Na wewe pia:
✅ Maandiko yapo juu yako
✅ Unabii umeandikwa
✅ Je, unajua?
✅ Umeyadai?
Umegoma kuyasoma.
Umegoma kuamini mwaka wa Bwana ulio amriwa juu yako.
Matokeo? Miaka inapita kama fast forward.
🎯 KUDAI ANDIKO
Kabla huja-claim neno lolote, lazima ulijue.
Na si kujua tu kwa kusikia, bali kulielewa na kulipokea.
Usicho kijua, huwezi kukidai.
Usicho dai, huwezi kukipokea.
Na usichopokea, hakikusaidii hata kidogo.
✅ FINISHED WORKS OF CHRIST
Yesu alikamilisha yote.
“It is finished!”
Ni kazi zako sasa:
-
Jua kilichokamilishwa.
-
Jua maandiko yako.
-
Yadai.
-
Pita katikati ya wanaokukataa.
-
Tangaza mwaka wa Bwana ulio amriwa juu ya maisha yako.
Kwa hiyo usikae kulia Nazareti ohhh walinikataa.
Usijieleze ovyo.
Usilazimishe kupendwa.
PITA KATI KATI YAO. UENDE ZAKO.
MAJIRA HAYAJAISHIA KWAO.
MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA UPO JUU YAKO.
CHAPTER 4 …..
Yesu anaenda kufundisha hekaluni siku ya sabato na watu wana mshangaa mnoo!, kwanini? Neno lake lilikuwa na uwezo mzito sana yaani Neno lake lilikuwa linanena.
Mpendwa Neno lilinena haswaa mpaka ndani ya hilo Sinagogi kulikuwa na mtu anapepo likashindwa kujishikilia kwa kuchomwa na lile Neno likalipukaa. Yesu analikemea lile Pepo lisimwage mchele kwenye kuku wengi likamharibia mingo zake mapema mapemaa.
Mpendwa uwezo wa Yesu ulikuwa impeccable to the extent watu waka staajabu ni neno gani hili leo analohubiri, si hilihili la kila siku??, Mbona leo mpaka pepo wana mtii?. Mpendwa hii ikwambie tu kuwa there is a way haupo serious na neno ndiyo maana changamoto zina kukaziaa hazipepesi kope.
There is something you are not doing right, rudia kusoma neno ukiwa umejizatiti. Yesu anamponya mkewe Simioni, anamkemea magonjwa nayo yana tii, after that anaenda kwenye healing spree!, anaponya watu back to back na anawatoa mapepo back to back!.
Unachotakiwa kutoka nacho leo kwenye hii chapter 4, ya Gospel of Luke ni kwamba uponyaji upoo na unaendelea kwa Bwana Yesu.
Maradhi yako, Affliction zako kama zimesababishwa na mapepo au nguvu za giza zitaponywaa kwa B Bwana Yesu. Jesus healed everything and he is still in the business of healing. Sawasawa na andiko hili nenda mbele zake msihi akuponye na hiyo changamoto sasa.Kesho meditate kipande hiki huku ukimsihi akuponye na hiyo changmoto yako.
LUKA 5
Yesu awaita wavuvi wafuasi wake
1 Ikawa makutano walipomsonga wakilisikia neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti;
2 akaona mashua mbili zimesimama kando ya ziwa; lakini wavuvi walikuwa wametoka, wakiosha nyavu zao.
3 Akaingia katika mashua moja, iliyokuwa ya Simoni, akamwomba aiondoshe kidogo kutoka puani; akaketi, akawafundisha makutano toka mashuani.
4 Alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, “Ondoa mpaka kilindini, mkazitupe nyavu zenu mvue.”
5 Simoni akajibu, akasema, “Mwalimu, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazitupta nyavu.”
6 Walipokwisha kufanya hivyo, wakapata samaki wengi mno, hata nyavu zao zikaanza kukatika.
7 Wakawapungia mikono wenzao waliokuwa katika mashua ya pili waje kuwasaidia. Wakaja wakazijaza mashua zote mbili, hata zikaanza kuzama.
8 Simoni Petro alipoona hayo, alianguka magotini pa Yesu, akisema, “Ondoka kwangu, kwa kuwa mimi ni mtu mwenye dhambi, Bwana.”
9 Maana mshangao umemshika, yeye na wote waliokuwa pamoja naye, kwa sababu ya wingi wa samaki walioupata.
10 Na vile vile Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, waliokuwa washirika wa Simoni. Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.”
11 Hata walipokwisha kuziingiza mashua pwani, wakaviacha vitu vyote, wakamfuata.
Yesu amponya mwenye ukoma
12 Ikawa alipokuwa katika mji mmoja, kumbe! mtu mmoja aliyejaa ukoma! Alipomwona Yesu, akaanguka kifudifudi, akamsihi, akisema, “Bwana, ukiwa na nia waweza kunitakasa.”
13 Akanyosha mkono wake, akamgusa, akisema, “Nataka; takasika.” Mara ukoma wake ukamwacha.
14 Akamwagiza asimwambie mtu; ila, “Nenda ukajionyeshe kwa kuhani, ukatoe sadaka kwa kutakaswa kwako, kama Musa alivyotoa amri, iwe ushuhuda kwao.”
15 Lakini habari zake zikaenea zaidi; makutano makubwa yakakusanyika kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
16 Lakini yeye alikuwa akijitenga akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba.
Yesu amponya aliyepooza
17 Ikawa siku moja alipokuwa akifundisha, Mafarisayo na walimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijiji cha Galilaya, na Yudea, na Yerusalemu. Uweza wa Bwana ulikuwapo ili awaponywe.
18 Na tazama! Watu walileta kitandani mtu aliyekuwa amepooza; wakatafuta njia ya kumwingiza wamweke mbele yake.
19 Na kwa sababu ya lile kundi la watu hawakuweza kumwingiza, walipanda juu ya dari, wakamshusha pamoja na kitanda chake katikati mbele ya Yesu.
20 Naye alipoona imani yao, alimwambia, “Ewe mtu, umesamehewa dhambi zako.”
21 Mafarisayo na waalimu wa torati wakaanza kuwaza, wakisema, “Ni nani huyu asemaye makufuru? Ni nani awezaye kusamehe dhambi ila Mungu peke yake?”
22 Lakini Yesu alitambua mawazo yao, akajibu, akawaambia, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
23 Lipo jambo lipi jepesi, kusema, ‘Umesamehewa dhambi zako’, au kusema, ‘Simama, utembee’?
24 Lakini mpate kujua ya kuwa Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi,” (akamwambia yule aliyepooza,) “Nakuambia, Inuka, jitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako.”
25 Mara akaondoka mbele yao, akajitwika kitanda chake, akaenda nyumbani kwake, akimtukuza Mungu.
26 Wote wakastaajabu, wakamtukuza Mungu; wakajaa hofu, wakisema, “Tumeona mambo ya ajabu leo.”
Yesu amwita Lawi
27 Baada ya hayo akatoka, akamwona mtoza ushuru jina lake Lawi, ameketi forodhani; akamwambia, “Nifuate.”
28 Akaacha yote, akainuka, akamfuata.
29 Lawi akamfanyia karamu kubwa nyumbani mwake; na kundi kubwa la watoza ushuru na wengine walikuwa pamoja nao mezani.
30 Mafarisayo na waandishi wao wakawanung’unikia wanafunzi wake, wakisema, “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?”
31 Yesu akajibu, akawaambia, “Wenye afya hawamhitaji tabibu, bali walio hawawezi.
32 Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi, wapate kutubu.”
Swali juu ya kufunga
33 Wakamwambia, “Mbona wanafunzi wa Yohana hufunga mara nyingi na kusali vivyo hivyo na wanafunzi wa Mafarisayo, bali wako hula na kunywa?”
34 Yesu akawaambia, “Mwaweza kuwafanya wana wa arusi wafunge, wakati bwana arusi yu pamoja nao?
35 Lakini siku zitakuja ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao, ndipo watakapofunga siku zile.”
36 Akawaambia mfano; “Hakuna mtu ashonae kiraka cha nguo mpya katika nguo ya zamani; hila hiyo mpya huchanika nayo, wala kiraka hicho cha mpya hakipatani na ya zamani.
37 Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vya zamani; vinginevyo divai mpya huvipasua viriba, divai hutiwa na viriba huharibika.
38 Lakini divai mpya yapasa kutiwa katika viriba vipya.
39 Wala hakuna mtu atakayekunywa ya zamani na mara kutaka mpya; kwa maana husema, ‘Ya zamani yatamu.’”
CHAPTER 5
Luka: 5 : 4 – 5
Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki. Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu, lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.
Kwa neno lako nitashusha nyavuu!, Wengi mmekwama eneo flani na mmeshajiwekea akilini hii ngori, hiki kipengele. Usiku wa leo bwana Yesu anasema shusha nyavuu hilo eneop acha mashaka, acha wasiwasi, acha woga!. Hata kama hilo eneo miaka na miaka unatokaga mweupe hupati kitu, Shusha nyavu acha kuogopa historia.
Mpendwa Andika/ ainisha eneo la maisha yako amabalo bila neno la Yesu nyavu hishushii. Deliverancve ya Gospel sio nyepesi,Inabidi leo usiku wote na kesho yote usimame na andiko hili kwenye hiyo changamoto yako siku nzima.
Luka: 5 : 5
Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu, lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.
Unamwambia bwana Yesu kwa neno lako nitaomba kazi tena, kwa neno lako nitajaribu tena biashara, kwa neno lako nita jaribu tena tena mahusiano, kwa neno lako nitajaribu tena uzao. You have to decree and declare this scripture all day tommorrow. Mpaka liingie moyoni mwako. The morev you declare the more utapata amani na deliverance ndiyo inafanyika.
Wapendwa isse ni ile ile faith yaani faith! and hope!. Unaweza kuwa una changamoto ndogo sana ila ika kubleed dry just because you don’t have faith, Na unaweza kuwa na changmoto kubwa lakini uka i-solve kwa imani ndogo sana.
Mpendwa watu wengi mnachanganya beleiving and wishing, Most of you just wish for things to happen, and Wishing is mere hopew that is baseless of nothing maybe just your imaginary hopes and delulu, no work is put behind the wish, no strategy, no plans whatsoever.
Like the saying goes delulu’s, not a solulu, Dlution is not a solution. Namwamini Mungu for a husband is not the same as I widh God will send me someone, Wapendwa most of you wish, ndiyo maana hata kusoma injili ni kazii!, kunfunga mdiyo kabisaa! kutoa sadaka ya ukombozi labda siyo wewe.
Ila maneno matupu sasa ya ‘Mungu nipe mume’ kama vote—na of course ni baseless kabisa katika scriptures. Just your own whinings and tatarums! Unaacha zinaa siku 2 ukiona Mungu yupo kimya, unarudi kuzini mwaka mzima alafu unatubu siku 3! Ikawa asubuhi, ikawa jioni, ikawa miaka 20 huna breakthrough eneo la ndoa.
Kuna watu niko nao kwenye deliverance—mtu ana miaka 7 hana mahusiano. Sio ajabu! Lakini ukimuuliza: “In those 7 years umefanya maombi gani exactly?”
“Ni maandiko gani ulikuwa umesimamia nayo?”
“Ni andiko gani umelishika kwa miaka yote hiyo hadi Mungu ajithibitishe?”
Miaka 7 umesoma maandiko gani? Vitabu vingapi vya Biblia umevimaliza?
Most times ni utopolo mtupu! Ufyoroo ufyoroo. Total nonsense! Na nikimuuliza mtu umefika elimu gani? Most atasema UDSM, hapo ndo na nikata maini.
Definately “wisdom is not freedom for you!” You have no wisdom whatsoever!
Ooh mimi naenda kuombewa kwenye makongamano! Unataka utoke kwako huna kazi eeh, urudi na kazi. Na hivi upentekoste umekuja na majahazi, basi tuna u-abuse kweli kweli!
Watu wananiona wananiuliza: “Mama mbona huombi kwa sauti sana?”
Najua wanamaanisha nini! Wanataka mtu anayehenya, anayelia hadi sauti ikauke, anayezungumza kwa lugha masaa 5 nonstop! Lakini usijidanganye — The approach is weak as hell and has no substance whatsoever! The wishers anthem!
Mtu kasoma vitabu 10 vya Biblia, kaja na njaa ya rohoni, kabatizwa kwa Roho Mtakatifu, si mbaya akiombewa au kutafutiwa direction. They earned it! Na hakuna kitu unaweza kumfundisha ambacho hajui tayari.
Lakini wewe? Hata kitabu kimoja cha Biblia hujasoma!
Unamaliza week hujasali. Ni mpagani uliyechangamka. Una-seek guidance ya Roho Mtakatifu ya nini?
Roho Mtakatifu huzungumza kupitia neno, na wewe huna neno hata robo ndani yako! Mnaongea nini? Mnaongea vipi?
Watu ninaowakuta kwenye deliverance ambao ni live Christians huwa wanavuka fasta!
Tulianza Agosti mwaka jana, mpaka sasa wengine wameshalipiwa mahari na wako kazini. Wale wa morning glory, safi sana! Neno linamiminika ndani yao. Magnificent!
Mtu ana neno, shida yake ni authority, unaikazia—imeisha!
Unaprophecy juu yake, reception yake ni solid. Fasta fasta mmemaliza. Mungu anajithibitisha kwa ukubwa.
Lakini wengine? “Mama, nipe unabii.” Kama sina lolote, naweza kusema: okay, I like you, so let me do you a favor. Na force unabii, nachomeka kwenye scripture halafu nakupatia.
BUT — can you receive it?
Thubutu!
SABABU HUJUI UNABII NI NINI. Kuna unabii wa aina ngapi? Unabii unafanyaje kazi? Degree unayo lakini you won’t even bother to find out!
Unataka kukimbia race kabla hujatambaaa.
Kumpa mtu kama wewe unabii ni kama kuji-shoot mguuni. Atasumbua kweli!
Mtu hana kazi, haendi kanisani, hatoi sadaka hata ya shilingi 10, hana ratiba ya ibada, hana desturi hata ya kuomba once a week!
Kusoma maandiko — aaah, ata washwa na upupu!
Na kama huna kazi, unaweza maliza Injili ya Luka siku 5. Ni vile una akili lakini huzitumii.
Believing in God means walking the path of the righteous—not because it’s simple, but because you want to please and obey God!
Unaacha zinaa sio sababu huna upwilu, bali kwa sababu unatii amri za Mungu.
Mungu ni Neno lake. Na usiposoma Neno, unamwamini Mungu yupi? Kama husomi maandiko, wewe ni mpagani kamili. Mungu hujifunua kupitia neno lake. Kama hulisomi, hamna lolote juu yako.
Mimi mtu akiniambia “niko kwenye waiting for 7 years” — I want to see scripts! Plans! Strategies! Executions!
Andiko gani umelisoma na kuli declare miaka 7? Sadaka gani umepeleka juu ya hilo andiko? Umefunga mara ngapi?
Umesoma vitabu vingapi vya Biblia?
Hii ndo intentional Christianity.
Hii ndo serious faith.
Wale wa deliverance waliokuja na akili zao timamu, miezi 3 tu — kazi imeisha. Kwanini?
Because faith executed properly has results.
Wale ndugu wa yule mtu aliyepooza kwenye Injili waliamua: Let’s get him to Jesus — that’s it!
They cut through the roof. Wakajitoa. Wakajua YESU ni mtu wa kazi hiyo.
Do you believe that Jesus is the man for your task?
Kwamba ukifika mbele za Yesu, kila lango linafunguka?
Kwamba kazi, ndoa, uzazi, kila kitu kinafunguliwa?
DO YOU REALLY BELIEVE IT?
Sadly, most of you stupidly don’t.
And yes, I used the word stupid!
I mean it. And I could say worse.
Unamuheshimu boss wako kuliko Yesu. Uko tayari kupendekeza kwa landlord kuliko kwa Roho Mtakatifu.
Zaka humtoi, lakini ukiona harusi ya rafiki umetoa laki 2!
Wewe ni cooked!
Unaomba kazi kwa Yesu ambaye hujasoma hata kitabu kimoja cha maisha yake.
Which Jesus? The one whose word you ignore?
Sis, you is cooked!
Na kazi yangu kama rafiki ya kweli ni kukubeba kama wale watu wa yule aliyepooza — kukufikisha mbele za Yesu leo hii.
Yesu siyo mwanadamu aseme uongo.
Mwanzo 2:24 — “Mwanaume atamwacha baba na mama yake, akaambatana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja.”
Full stop!
Scripture iko!
Huna haja ya kiraruu raruuu.
Declare that word!
Decree it!
Live it!
Sadaka zako zipitie kwenye hilo neno!
Funga kwa hilo neno!
Tembea nalo miaka 7 kama linauhusiano na maisha yako. Simamisha neno juu ya maisha yako.
If you say you believe in God for a husband for 7 years, then let it show!
Sadaka zako ziongee! Scripture zako ziongee! Declaration zako ziongee! Funga zako ziongee!
Usiruke-ruke kama kuku aliyetoka kwa kichinjio!
Mama ndoa! Mama ndoa!
But you don’t even believe in the scripture that speaks about it.
Kwa kumalizia…
Mimi ni kama wale rafiki wanne wa yule mtu aliye pooza.
Nakubeba leo!
Na kwa nguvu zote ninakufikisha mbele za Yesu!
Na ninakuambia mbele za macho yako:
“Yesu ni mtaalamu wa mambo yako.”
Kama unamwamini kweli, utapona. Utafufuka. Utaolewa. Utafanikiwa.
BUT FIRST — repent of your unbelief.
Tubu dhambi zako. Tubu kiburi chako. Tubu uvivu wako wa kusoma neno.
Na ukae kitako — usome Biblia. Simamia neno. Declare kila siku. Funga. Toa sadaka. Jenga altar. And then, watch God show up.
Mengine ni kelele tu. Na mungu haulizwi na kelele.
CHAPTER 5 ….
Watu wengi mnajaribu kuwa na mahusiano ya ghafla sana na ya zimamoto na Yesu ndiyo maana hayafiki popote. Jesus is very very different na manabii wengine na manabii wengine wote na mitume huwezi kutengeneza uhusiano wa ghafla sana na bwana Yesu from no where, Yani interview kesho leo ndiyo ujibalaguze Yesu wangu, Yesu wangu! wala havita swii! utaenda na utakosa hiyo kazi vizuri tu.
Bwana Yesu is more of longterm friend, ni mtu amabaye ukianza kujenga uhusiano neye leo unaweza usione chochote yamkini ukajiona chizi kabisaa ila he will appear when you need him most and you will know it is Jesus, Ndiyo maana watu wengi wa kuzuga zuga hawafaulugi.
Sisi tulio kwa Yesu tulikuwa luba tuu ndiyo siri ya mafanikio unaweka ratiba ya saa 9 unasali na hamna jipya na kesho una sali tena, kama hapa tupo chapter 5 tuna ua na Yesu yupo kama hayupo ila ipo siku uanishukuru.
Tofauti ya Yesu na mitume wengine na manabii? Veve alitoka kwa Baba na alimjua Baba na alichokifanya haikuwa guess works.
Manabii wengi ne hawakumjua Mungu kama Musa… katika kumsihi Mungu asiwaangamize wa Israeli mlimani, kashuka kayeyusha dhahabu zao zoteee za miungu na kuwanywesha kuanzia katoto ka miaka 3 mpaka mzee wa miaka 100 plus. That was NOT God’s way!
Nabii Elia kaambiwa nenda kajionyeshe kwa mfalme naleta mvua. Veve akaona sasa ni muda muafaka wa veve ku-settle score na Baal na manabii wake. Haiwezi mvua kuja wakati hawajamalizana! Veve sio wa kuteseka njaa afu mambo yaishe kirahisi. What does he do next? Calls fire from heaven! Commits mass murder and massacre of all Baal’s prophets! Na walikuwa 400! He made sure he murdered all 400 prophets.
Elisha? Couldn’t take a joke from young boys! Cheko kidogo kawaitia dubu wakawaua vijana wote. Kwishaaaa! Just for laughing at his upara.
Manabii wa sasa wanatenda sana dhambi? Mmmhhh! Labda kuendekeza ukware tu na njaa.
Elisha time of famine? Watu wanakula watoto wao. Na zilikuwa sio shida zakeee! Mpaka mfalme akaamua “yuko wapi yule Nabii Elisha nimchinjeee mwenyewe!” Popote nitakapokutana naye ijulikane moja kwamba Israeli hatuna Mungu wala nabii!
YESU – A DIFFERENT KIND OF PROPHET
Yesu was very, very different! Njia zake mpaka leo si za kupelekeshana na mikwaraaaa! Sio za kutishana na kuweka mtu mguu wa shingoni. Jesus was a cool prophet. A little too cool for the Jews liking.
Kama hapo alikuwa ana vibe na watoza ushuru kwenye liparty lao! Ana jiachiaaaa na wezee wa tozoooo! You may not understand whyyy? Because Jesus was all about people and their personalities not their sins.
Interaction zake na watu zilikuwa based on WHO they were, not WHAT they had done. Kama Lawi! Eventually Mathayo. Hakuwa na tabia ya ku-label watu! “Nyie wazinzi wakubwa!” “Nyie walevi!” Never that.
YESU ANAEPUSHA MAWE, SIO KUPIGA MAWE
Hata yule mwanamke aliyekutwa LIVEEEEEEE anatoa mzigo! Ushahidi kamilika! Lakini Yesu bado anakataa kumuita jina la dhambi yake. Him being Jesus watu walitegemea angemchapa bakora sio chini ya 20 na mawe 30. But nope! He acquitted her. Forgave her. And warned her.
Watu wengi tunashindwa kwenda kwa Yesu sababu ya dhambi zetu! Tunaona ni kinafiki mno. Tunaweza pigwa hata radlll. Maana kama janaba badooo bichlll kabisa.
DHAMBI HAIKUACHI – YESU NDIO MSAADA
Wengi mnajidanganya. Unataka kuacha zinaa ndo uje kwa Yesu. NO! You will never leave sin unless Bwana Yesu akusaidie. It’s human nature! You will feel upwiruuu if your reproductive system is okay!
Hata ukiingia ndani ya ndoa — wembe ni ule ule. Wembe wa ndoa ni laser! Si wax! Unaamka na huyo huyo miaka 5 — linakuchoshaaa! Ndani ya ndoa kuna majaribu mabaya kuliko uko nje. Maana viposongo vipyaaaa vina pull attention kuliko pilimzuzu wako mwenye mikojo ya Osama Bin Laden!
USIACHE YESU KWA AJILI YA NYAMA YA MWILI
Kitu pekee kitakacho kufanya usizini si kuwa umekosa upwiruu, ni kuwa na relationship thabiti na Yesu. Relationship ambayo ulichukua miaka 3 kuijenga. Umebatizwa kwa Roho. Unatembea kwenye dominion. Huwezi kuivunja kizembe tu.
Kama uhusiano wako na Yesu ni wa uzlll fasta – utafall! You can’t survive with a Jesus you barely know.
JESUS IS NOT YOUR EMERGENCY BUTTON
Yesu hataki uhusiano wa msibaaaaa. Yaani unamtafuta tu mambo yakiharibika! You must be intentional! You and Jesus time kila siku. Lisaa li moja – Non-negotiable. Soma Injili. Tafakari. Learn the Jesus of the gospels!
Talk to Him about everything. Wins! Losses! Goliaths! Mpe kila kitu. Wekeza ku-mjua Yesu! Kama huwekezi, usitarajie breakthrough za million 10!
SIKU MOJA YA YESU NI BORA KULIKO AJIRA YA UJINGA
Unaacha kazi ya manyanyaso ya laki 8 kwa imani. Wakikubeza — wewe jibu:
Romans 3:4
“Let God be true, and every man a liar…”
Sawa, utasota miezi 6. But when the door opens, utashinda wote waliokukejeli. Hata wazazi wako watasema “Flani ana Mungu yuleeeee!”
THIS GENERATION? FOOLISH!
Watu wanauza maadili yao sababu ya njaaaa. Umepewa akili timamu! Ukikataa kazi ya manyanyaso unaitwa “kichaa”! Lakini akili yako inajua Yesu hawezi kukuacha hivyo!
Holy Spirit akikupa prophecy — anatoa strategy pia! Kama hujui wapi pa kuipata, hujawekezwa kwenye mahusiano. Ndo maana wengi ne mpo clueless. Na mnaomba kazi za million 10 bila Holy Spirit. Thubutuuuuuu!
JESUS WANTS ALL OF YOU!
Bwana Yesu anataka if you win, you win together! If you lose, you lose together. Kama kuchanganyikiwa — uchanganyikiwe ndani ya Kristo!
You don’t show weakness. You rise in the face of chaos declaring:
“Nayaweza yote katika Yeye anitiaye nguvu!”
“Giza halijawahi kuishinda Nuru!”
Mshahara wa laki 8? Sipokei!
Million 10 ama nothing!
“Mungu wangu ni Mungu wa million 10 minus nothing!”
YOUR VICTORY IS IN INTENTIONALITY
Ukikaa na Yesu, usome Injili, umtafakari kila siku — utaona matokeo!
Mpaka wale waliokubeza watasema,
“Nyieeeee! Huyu ana Mungu!”
Yesu ni Bwana wa harusi, si wa misiba! Huwezi kumjua kwenye vilio tu! Jua Yesu kwa hali zote.
YESU TU! SIO HOKO KUKIMBIAKIMBIA!
Unataka ndoa? YESU.
Unataka kazi ya maana? YESU.
Unataka kusimama imara kwa usafi wa moyo na mwili? YESU.
Usitumie mafuta. Usilale kwa watumishi. Usikimbilie mimba.
Find JESUS. Build with Him. Walk with Him. Decree His word.
Weka mkutano na Roho Mtakatifu na utoboe.
When Holy Spirit gives prophecy — He gives strategy!
Without relationship, you’re chasing shadows.
LUKA 6 (Biblia – Kiswahili Union Version)
1 Ikawa siku ya sabato alipokuwa akipita katika mashamba ya nafaka, wanafunzi wake walikuwa wakivunja masuke, wakayapukusa mikononi mwao na kuyala.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Mbona mnafanya jambo lisiloruhusiwa siku ya sabato?”
3 Yesu akawajibu, “Huku mmesoma alilofanya Daudi alipokuwa na njaa, yeye na wale waliokuwa pamoja naye?
4 Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, akatwaa ile mikate ya onyesho, akala, akawapa na wale waliokuwa pamoja naye, ambayo haikuruhusiwa kuliwa isipokuwa na makuhani peke yao?”
5 Akawaambia, “Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.”
6 Ikawa siku nyingine ya sabato aliingia katika sinagogi akafundisha. Na pale kulikuwa na mtu mkono wake wa kuume umepooza.
7 Waandishi na Mafarisayo wakawa wanamvizia, ili waone kama ataponya siku ya sabato, wapate sababu ya kumshtaki.
8 Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Simama usimame katikati.” Akaondoka akasimama.
9 Kisha Yesu akawaambia, “Nauliza, je, ni halali siku ya sabato kutenda mema au kutenda mabaya? Kuokoa maisha au kuua?”
10 Akawatazama wote pande zote, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Akaunyosha, mkono wake ukapona.
11 Lakini wao wakajaa hasira, wakaanza kushauriana wao kwa wao juu ya kumfanya Yesu nini.
12 Ikawa siku zile alienda mlimani kuomba, akakaa huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13 Kulipopambazuka aliwaita wanafunzi wake, akachagua kumi na wawili miongoni mwao, akawaita mitume:
14 Simoni, ambaye pia alimwita Petro, Andrea nduguye, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo,
15 Mathayo, Tomasi, Yakobo wa Alfayo, Simoni aitwaye Zelote,
16 Yuda wa Yakobo, na Yuda Iskariote ambaye baadaye aligeuka kuwa msaliti.
17 Akashuka pamoja nao, akasimama mahali tambarare, pamoja na wafuasi wake wengi na umati mkubwa wa watu kutoka Uyahudi wote, Yerusalemu, na pwani ya Tiro na Sidoni, waliokuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
18 Na wale waliokuwa wakiteswa na pepo wachafu waliponywa.
19 Na umati wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa ikitoka kwake na kuwaponya wote.
MAHUBIRI YA YESU NA BARAKA NA LAANA
20 Akayainua macho yake, akawaangalia wanafunzi wake, akasema:
“Heri ninyi mlio maskini, kwa kuwa Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Heri ninyi mnao njaa sasa, kwa kuwa mtashiba.
Heri ninyi mnaolia sasa, kwa kuwa mtacheka.
22 Heri ninyi watu watakapowachukia, na kuwatenga, na kuwatukana, na kuwatupilia mbali kama waovu kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
23 Furahini siku hiyo na kurukaruka kwa furaha, kwa maana tazama, thawabu yenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana baba zao waliwatenda manabii mambo kama hayo.”
24 “Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, kwa kuwa mmekwisha kupata faraja yenu.
25 Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, kwa kuwa mtapata njaa.
Ole wenu mnaocheka sasa, kwa kuwa mtaomboleza na kulia.
26 Ole wenu watu wote watakaposema mema juu yenu, kwa maana baba zao waliwatenda manabii wa uongo mambo kama hayo.”
UPENDO KWA MAADUI
27 “Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukia,
28 wabarikini wale wanaowalaani, waombeeni wale wanaowaonea.
29 Mtu akupigaye shavu moja, mgeuzie na la pili; mtu akikuondolea joho, usimkataze na kanzu.
30 Mpe kila akuombaye, na mtu akikuondolea mali yako, usimrudishie.
31 Na kama mnavyotaka watu wawafanyie ninyi, vivyo hivyo na ninyi fanyeni wao.
32 “Kwa maana mkipenda wale wanaowapenda, mna faida gani? Maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda.
33 Nanyi mkifanya mema kwa wale wanaowatendea mema, mna faida gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo.
34 Nanyi mkikopesha kwa wale mnaotumaini kupata kwao, mna faida gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi, wapate kulipwa sawasawa.
35 Lakini wapendeni adui zenu, fanyeni mema, na kukopesha bila kutumaini kurudishiwa; na thawabu yenu itakuwa kubwa, nanyi mtakuwa wana wa Aliye Juu, kwa kuwa yeye ni mwema kwa wasio na shukrani na waovu.
36 Basi iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
USIHUKUMU
37 “Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa. Msilaumu, nanyi hamtalaumiwa. Sameheni, nanyi mtasamehewa.
38 Toeni, nanyi mtapewa. Kikapu kizuri, kilichosukwasukwa, kimejaa na kusukwa juu, watakipimia vifuani mwenu. Kwa maana kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.”
39 Akawaambia mfano pia: “Je, kipofu aweza kumwongoza kipofu? Je, hawa wote wawili hawataanguka shimoni?
40 Mwanafunzi hampiti mwalimu wake; lakini kila aliye mkamilifu atakuwa kama mwalimu wake.
41 Mbona waona kijiti kilicho katika jicho la nduguyo, na huoni boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42 Au wawezaje kumwambia nduguyo, ‘Ndugu, acha nikitoe kijiti kilicho jichoni mwako,’ nawe huoni boriti iliyo katika jicho lako? Mnafiki, toa kwanza boriti katika jicho lako, ndipo utaona vizuri kutoa kijiti kilicho katika jicho la nduguyo.”
MTI MZURI NA MATUNDA MAZURI
43 “Kwa kuwa hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri.
44 Kila mti hujulikana kwa matunda yake. Kwa maana hawachumi tini katika miiba, wala hawavuni zabibu katika michongoma.
45 Mtu mwema hutoa mema katika hazina njema ya moyo wake, na mtu mwovu hutoa mabaya katika hazina mbaya; kwa kuwa mtu hunena yatokayo katika wingi wa moyo wake.
KUJENGA JUU YA MISINGI IMARA
46 “Mbona mnaniita, ‘Bwana, Bwana,’ wala hamfanyi nisemayo?
47 Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu, na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake:
48 Ni kama mtu ajengaye nyumba, akachimba chini sana, akaweka msingi juu ya mwamba; palipotokea mafuriko, mto ukapiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa juu ya mwamba.
49 Lakini asiyesikia na kutenda ni kama mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi bila msingi; mto ukapiga nyumba ile, nayo ikanguka mara, na maangamizo yake yakawa makubwa.”
Luka 6
1 Ikawa siku ya sabato alipokuwa akipita katika mashamba ya ngano wanafunzi wake walikuwa wakivunavuna masuke, wakayala, wakiyapukusa kwa mikono yao.
2 Wafarisayo wengine wakasema, Mbona mnafanya yasiyofaa siku ya sabato?
3 Yesu akajibu akawaambia, Hamkusoma hata aliyoyafanya Daudi alipokuwa na njaa, yeye na wale waliokuwa pamoja naye?
4 Jinsi alivyoingia nyumbani mwa Mungu, akatwaa ile mikate ya onyesho, akala, akawapa na waliokuwa pamoja naye, ambayo haikupasa kuliwa ila na makuhani peke yao?
5 Akawaambia, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.
6 Ikawa siku ya sabato nyingine aliingia katika sinagogi akafundisha; na pale alikuwepo mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 Waandishi na Mafarisayo walimvizia, waone kama ataponya siku ya sabato, wapate sababu ya kumshitaki.
8 Lakini yeye alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, Inuka usimame katikati. Akaondoka akasimama.
9 Yesu akawaambia, Nawauliza ninyi, Je! Ni halali siku ya sabato kutenda mema au kutenda mabaya? Kuokoa maisha au kuua?
10 Akawakazia macho wote akamwambia, Nyosha mkono wako. Akafanya hivyo, mkono wake ukarudi kuwa mzima.
11 Nao wakajaa wivu wakaongea wao kwa wao walitafanyaje Yesu.
12 Ikawa siku zile akatoka akaenda mlimani kuomba; akakesha usiku kucha akimwomba Mungu.
13 Hata kulipopambazuka aliwaita wanafunzi wake, akachagua katika wao kumi na wawili, aliowaita Mitume;
14 Simoni ambaye alimpa jina la Petro, na Andrea nduguye, na Yakobo, na Yohana, na Filipo, na Bartholomayo,
15 na Mathayo, na Tomasi, na Yakobo wa Alfayo, na Simone aitwaye Zelote,
16 na Yuda wa Yakobo, na Yuda Iskariote aliyekuwa msaliti.
17 Akashuka pamoja nao, akasimama mahali tambarare, pamoja na wingi wa wanafunzi wake, na mkutano mkuu wa watu waliotoka Uyahudi wote, na Yerusalemu, na pwani ya Tiro na Sidoni, waliokuja kumsikia na kuponywa magonjwa yao;
18 na wale walioteswa na pepo wachafu waliponywa.
19 Na mkutano wote walitaka kumgusa, kwa kuwa nguvu ilitoka kwake wote wakaponywa.
20 Akainua macho yake akawatazama wanafunzi wake, akasema,
Heri ninyi mlio maskini, kwa sababu Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Heri ninyi mnaolilia sasa, kwa kuwa mtacheka.
Heri ninyi mnaoona njaa sasa, kwa kuwa mtashiba.
22 Heri ninyi watu watakapowachukia, na kuwatenga na kuwahukumu, na kuitupa nje jina lenu kama ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
23 Furahini siku ile, mkashangilie; kwa kuwa tazama, thawabu yenu ni kubwa mbinguni; maana baba zao waliwatenda manabii vivyo hivyo.
24 Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri! Kwa sababu mmeipata faraja yenu.
25 Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa! Kwa kuwa mtaona njaa.
Ole wenu ninyi mnaocheka sasa! Kwa kuwa mtaomboleza na kulia.
26 Ole wenu watu wote watakaposema mema juu yenu! Maana baba zao waliwatenda manabii wa uongo vivyo hivyo.
27 Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukia.
28 Wabarikini wale wawaalaani, waombeeni wale wanaowaonea.
29 Mtu akupigaye shavu moja, mgeuzie na la pili; na mtu akuondoleaye joho, usimzuie na kanzu.
30 Mpe kila akuombaye; na mtu akikuondolea vitu vyako, usimtake akurudishie.
31 Na kama mnavyotaka watu wawatendee ninyi, nanyi watendeeni vivyo hivyo.
32 Na mkiwapenda wapenzi wenu, mna fadhila gani? Kwa maana na wenye dhambi huwapenda wapenzi wao.
33 Na mkiwatendea mema wale wawatendeao mema, mna fadhila gani? Kwa maana hata wenye dhambi hufanya hivyo.
34 Na mkikopesha kwa wale mnaotumaini watarudisha, mna fadhila gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi, wapate kulipwa vile vile.
35 Bali wapendeni adui zenu, tendeni mema, na kukopesha bila kutarajia kupata malipo; na thawabu yenu itakuwa nyingi, nanyi mtakuwa wana wa Aliye juu; kwa kuwa yeye ni mwema kwa wasio na shukrani na waovu.
36 Basi iweni na rehema, kama Baba yenu alivyo na rehema.
37 Msihukumu, wala hamtahukumiwa; msilaumu, wala hamtalaumiwa; achilieni watu huru, nanyi mtaachiwa.
38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kiasi kizuri, kilichoshindiliwa, kilichotikiswa, kinachofurika, watamwangia vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa.
39 Akawaambia mfano, Je! Kipofu aweza kumwongoza kipofu? Je! Wote hawataanguka shimoni?
40 Mwanafunzi hampiti mwalimu wake; lakini kila mtu atakapokamilika atakuwa kama mwalimu wake.
41 Mbona wajitia kuchungulia kijiti kilicho jichoni mwa nduguyo, na boriti iliyoko jichoni mwako mwenyewe huiangalii?
42 Au wawezaje kumwambia nduguyo, Ndugu yangu, niache nitoe kijiti kilicho jichoni mwako, na wewe mwenyewe huioni boriti iliyoko jichoni mwako? Mnafiki! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, ndipo utaona sawasawa kulitoa kijiti kilicho jichoni mwa nduguyo.
43 Kwa kuwa hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya; wala mti mbaya uzaao matunda mazuri.
44 Kwa kuwa kila mti hujulikana kwa matunda yake. Maana watu hawachumi tini katika miiba, wala hawavuni zabibu katika kichaka.
45 Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema; na mtu mwovu katika hazina mbaya hutoa yaliyo mabaya; kwa kuwa mtu hunena yaliyomo moyoni mwake.
46 Mbona mnaniita, Bwana, Bwana, wala hamfanyi nisemayo?
47 Kila mtu ajaye kwangu, na kusikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonesha mfano wake mtu huyu ni mtu wa namna gani.
48 Mfano wake ni wa mtu ajengaye nyumba, aliyeyumba chini akachimba chini sana, akaiweka misingi juu ya mwamba; na palipokuja gharika, mto ukaipiga nyumba ile, haukuweza kuitikisa; kwa sababu imejengwa vizuri.
49 Lakini yule asikiaye lakini asiyetenda, ni mfano wa mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi pasipo msingi; ambayo mto ulipoipiga mara ikaanguka; maangamizo ya nyumba ile yakawa makubwa.
CHAPTER 6
Wapendwa kama nilivyo waambia Jesus is so different than all other major and minor prophets, He was all for the people not traditions. Yesu alikuwa na wanafunzi wake na wamechoka hasaa, anavunja desturi za kiyahudi for his people na alikuwa na options mbili aangalie traditions au watu, na akachagua watu like always.
Jesus always so the best in people ndiyo challange kubwa aliyotuachia, kuona mema katika watu regardless, if they are not even trying, regardless how imperfect they are.
People are not perfect and never will be, People will always be people, Yesu aliona wanafunzi wanaendekeza njaa kuliko Sabato!, It’s not like Jesus gave them the green light sasa jinomeni masuke hayoo mtakavyo, mjijambie, Hapanaa! wanafunzi walijichetua na Yesu aka ignore..
Mafarisayo walitegemea Yesu ndo awe mstari wa mbele kukemeaaaa uroho na ulafiii!
Lakini Yesu so the best in people kwamba wale sio waroho na walafi, ila njaa tu ndo imewazidi. Aka waachia watulize njaa zao… After all, veve ndo alikuwa ana wapigisha mzigo back to back. 😤😤®️!
Mafarisayo ni kama wengi wetu…
We will NEVER see the good in people! Neverrrrrr!
Mtu atafanya mema mia moja, ila tutabeba balaa moja hadi kaburini. We don’t give second chances. We don’t give room for growth. Judgement is our full-time ministry.
Na kama Mafarisayo, tunatumia maandiko au morals kujustfy hukumu zetu. “Amefanya au hajafanya?”
Let me spill…
Kuna ndugu yetu alienda kwa mume wa dada yake akiwa na miaka 19. Ilibainika ametembea naye. Dada yake maybe 30, mume wake maybe 40s. Sasa hapo wa kulaumiwa ni nani?
Mtoto wa miaka 19 au jitu la 40 lina itafuta 50?
It’s over 10 yrs now. Yule binti yupo kwenye 30s, but bado hapokelewi mahali popote kwenye “wanaume wa watu.” Na ni mtu wa upendo sanaaaa. Lakini watu zimeshika bango!
Even serikali inaangalia mtu alitenda kosa akiwa na umri gani! Sio sisi.
At 19, I don’t even think she knew the gravity of what she was doing. And she never even benefited from the sin!
We play God. And we lose!
Mtu alikukosea miaka mitano iliyopita? Basi roho inalo!
“Mimi sitaki mahusiano na toxic people!”
Asha alinifanyia hivi, basi SHOBOKA KWENDA ZAKO. Tuna choma madaraja bila kusita.
But guess what?
Yesu hakuwahi kumjudge mtu.
Aliona mema. Na hata alipokemea, alifanya hivyo kwa hekima na huruma.
Hakuwahi beba bango: “Weeee, nyaku nyaku! Mchawiiii!”
Me? I was naturally born rude!
Sisahau jamboooo! Roho ya kusamehe sinaaaa! Mtu wa vinyongo hatarllll.
Heshima naitaka dada!
Usipo nipa, naichukua kwa nguvu. Sitoi second chance.
Unanifanyia unafiki? BYEEEEE!
Na haya yoteeee ndo yalinifanya nisifike popote kwenye maisha yangu.
Shetani alinijulia mapungufu.
Akaanza kunipa kamba najinyonga mwenyewe.
Alipoona mtu anaweza kuwa destiny helper wangu, alimtumia kunisema.
Maneno hayana maana? Nitachoma daraja!
Ntakuita mbwa! Ntakushushia maneno kama gas cooker ya Kariakoo!
Important connections? I lost them all!
BUT GOD… 🙌
Niliokoka. Nikabatizwa kwa Roho.
Na nikaanza kuona tofauti…
Nimevaa ngozi ya KOBE.
I play the fool’s card!
Najipeleka matekaaaaa. Na imenilipaaaaa! 🙏
Sasa hivi?
Nawapa watu nafasi ya pili, ya tatu, ya tano!
I never give up on people.
Najua biashara ni uwanja wa unafiki — penye riziki hapakosi vita.
Lakini najichoma kama kubwa jinga.
And it works for me!
Hood wisdom…😎
Watu wananijua.
I’m from the hood.
Na reward disloyalty HAAAAAANDSOME.
Ukinitunza, nakutunza.
Ukini betray, na smile. Ushahidi unajitosheleza?
I still smile.
Wanakaa wakidhani nitatibuka, na mimi nachoma shoo kama haijaja kwa specs.
Nachekaaa. Kama KUBWA JINGA.
Wanakata tamaa.
Na wakija kuni-confront?
Nawajibu: “I heard, but sikudhani kama ni hivyo. Maybe mlichosema ni opinion yenu by then. I took that info to show you more good in me.”
Mambo yameisha!
Key: Be the big fool. It’s a winning card.
Huu mji ni mgumu.
Connections ni kila kitu.
Ukitaka kuingia kwenye cycles, lazima mtu wa damu na damu akutambulishe.
Mungu akaniinua kupitia rafiki wa kishua.
Mi nilikuwa low, yeye high.
Hakuwahi nifanya nijisikie mnyonge.
Tulienda China, akani kopesha, akanidhamini…
Mpaka biashara yangu ikasimama!
Baadaye, viwavi jeshi wakachomeka.
“Mtu huyo anakua sababu analoga!” 😳
Na watu wakaanza kunisema kila mahali.
Mama akaniambia:
“Nenda kajipendekeze. Usipoenda, nitaenda mimi mzazi wako!”
Nilijitoa kimasomaso.
Nilienda. Nika act kama Kubwa Jinga mbele yao.
Wakaona hawajaniweza.
Na rafiki yangu mpaka leo anafungua milango kwa ajili yangu.
Na yule aliyesema namloga? Leo ananitafuta mimi!
HAKUNA ALIYEKUWA MJINGA KAMA MIMI — na ndio maana MUNGU alinisafisha!
Final wisdom: DON’T PLAY GOD.
Ukienda kisheria sana, utaishia peke yako.
Relationships need grace.
Zikikosewa, kumbuka mazuri zilizokuwa nazo.
Opportunity cost ya kuvunja urafiki ni kubwaaa!
Usikunjie boss uso kama jino limevunjika!
Cheka. Bebea begi.
Show up early, go the extra mile — prove him wrong.
Unapenda mtu?
Usitake apite bila mapambano.
Sio kwa kugombana, bali kwa kuprove you’re the right one.
Men consider options — kama wewe unavo consider pia.
Don’t be bipolar.
Ukipata mwanaume mzuri, JITOFautISHE na visorokokwi wengine.
Usikate tamaa mapema — Dhoruba ni FURSA.
Umeachwa juu ya “hajibu message”? Kudadadekizenu!
Maybe ni kipindi.
Na wewe ndo ulikuwa nafasi sahihi, lakini ukaanzisha vita over nonsense!
Unataka ndoa?
Kaa kimya.
Teka mji.
Tumia fool’s card.
Watakukubali, watakuonea, lakini mwishowe watasema — huyu dada, ni mrembo na mwenye akili ya kushinda.
🎯 LESSON: Play the fool. Love big. Forgive hard.
Na usicheze nafasi ya Mungu.
Jesus never judged. Na wewe usijifanye God.
Grow. Learn. Love. SMILE kama Kubwa Jinga! 😎
Nikitakie neema ya kubeba roho ya kustahimili kama ya Yesu.
Kuna nguvu katika kusamehe na kunyamaza.
There is promotion in looking foolish.
KUBWA JINGA WINS.
CHAPTER 6…
Wapendwa people who don’t like you yaani hwahitaji sababu za msingi, This I learned the hard way in life, Usipojua utahangaika sana lakini ukijua utaishi kwa amani sana, sasahivi nikijua mtu ananichukia najiuliza tu nimemkosea nini?, What did I do to them?, kama hakuna basi wakafie mbele.
Wapendwa hiki kitu nimejifunza kwa Yesu, there was nothing bad he was doing to anyone ila hata wema mwingi alio utenda ulimuongezea maadui wapya kila siku. The guy only wanted to be good. Kuna mtu aliniambia nimetenda mabaya mengi yamenirudi nataka nibadilishe upepo nitende tende mema you know yaani kujitakasa tu!, Nikasema moto wa huku niwa gas maana unao watendea mema ndiyo wanakulipa ubaya ubwela, maumivu yake ni mara 1000 zaidi.
Wengi wetu dhambi nyingi tunatenda under the influence of people.Unawaza watu watasemajee?, Like any good has ever come from people. Wapendwa single mother wengi wa kwetu unashangaa, she can’t resist any change ya kumuachia mtoto, unaona kabisa she was not ready for a baby! wala hajatamani mtoto wala chochote.Unamuuliza kwanini umezaa under age 7 ooh!, Niliona mwanaume anatamani mtoto nimzalie, foolish little girl and poor baby maana wazazi madish yameyumba.
Na sio single mother tu msisimamishwe mishipa ya shingo hata wanawake sisi unakuta mtu mzima kabisaa, unataka ustaafu kumegwa kiselaa, unawaza i am for christ sake!!, How can I pull a no sex untill marriage??. I have been to the labor room 3 times for 3 men how can I pool a no sex till marriage?, I don’t wanna sin, truly I don’t God knows it, The devil knows it bt my past is conflicting me.
Wapendwa hata kazini umbea umbea haupendi wala majungu sio tabia zako lakini you like money, You like kupewa safari, you like promotions, you like soft life, so you sell your soul to the Boss to the enhance your career growth. You snich on ever living soul, Ikibidi kutembea na Boss wako sio shida zako anything to break the generational curse by sleeping your way the top.
Unaharibu na kuchezea hatma za wenzio kazini kama mdakoo wa kupanda chuki na uharibifu wa kuhakikisha hawaendi popote labda kama umekatika ulimi na hata kama umekatika ulimi you can still write an email labda uwe six feet under their only hope.
Most of you lazy women!! linerated free spirited kama ingekuwa hamna scrutiny! ndoa sio mambo yenu ni independent women lakini sababu ya voimdomo domo vya waja mnataka kuolewa not because it is your call rather to shut the hell up thy people. Unataka ndoa to rub it in their faces kwamba ukitaka ndoa unaipata.
Unakuta mtu yupo in her late 20’s already doing the mighty wonders, ana stable career already earning 5 million and above!, amejenga nyumba ana gari new model la million 60 kwenda juu. she is going to the top, dalili ya mvua ni wingu na tayari limetanda jeusii.
Anaanza kuhadaika na ndoaa!, Sisi tunamwambia you don’t need ndoa you need to find your soulmate, You have earned yourself and you officially afford to find love.Tafuta mtu ambaye mtapendana ataku-elevate kufika ule ukuu Mungu aliokukusudia.Anauliza mbona nyie hamkufata ushauri wenu?, Mpee! fosi ndoa uone kilichomtoa nyoka pangoni.
Akipigwa matukio mwezi tu ndani ya ndoa anakonda kama ka katautumbo. One year in the marriage, she has lost in her job muda wote anawaza amemkosea nini Mungu kikubwa hivyo to deserve son of the devil as a husband, hajali tena kuhusu kazi na kampuni inaona pale kwake ilijichanganya big time.
Anakuwa misarable all her remaining life anaishi na mtu amabaye hamopendii, huyo mtu wala huyo mtu hampendii. Hana amani ya Moyo maana anajiuliza aliishiaje hapoo?, akiondoka ndiyo ana watoto wawili tayari. Kazini ashaingia gundu.
Anarudi kutuuliza nyie mmewezaje ku-survive na kutoka on top of the things?, I’m sinkoing! aah sahivi ndiyo unataka ushauri? vumilia mtoto wa kike jikaze ki-kike! ushakosea hesabu upo kwenye lose lose situation, you can win by losing. Wewwe huwezi sababu you are not a foolish girl na hakuna jambo gumu kama mwanamke mwenye akili ku-play foolish,utapasuka sababu kila kitu unakiona waziwazi unakuwa mjinga vipi sasa?, una IQ kubwa hamna detail hutaiona.
Na worse enough you have your own mind, hauwezi kushikwa akili, wenzio tukiwaambia ruka kushoto as long as tumesema sisi na wanatuamini wataruka kushoto as long as tumesema sisi na wana tuaminix, wataruka kushoto hata akili yao iki challange vipi neno letu ndiyo watalifanya.
Any man can be tamed by any woman, she just needs to know the rules and play ny the rules and the rules are hard but bibi zetu waliweza ndiyo maana kila mwanaume alikuwa mume na talaka zilikuwa hamnaa.The golden rule was be really stupid to the stupor ukiweza add being foolish on top, sasa wanawake wenye akili hawezi, abadad asilani.
Watoto wa Magomeni anayeforce ndoa akiambiwa mjingaa wee! anasema ni kweli mume wangu, mimi mjinga kabisaa hadi familia yangu wajinga!. Huna akili kabisaa, ni kweli mume wangu wewe ndiyo mwenye akili kwa muda aliyopanga kuitumikia ndoa kabla haja wapurusaa mpaka vijiko akija kujifidia, kwenye talaka anafanya lolote muda wowote, Mpaka wakwe wanakuwa fooled, kumbe wenzao yupo on mission impossible on how to become rich by working smart and not hard.
Mtu akienda kuforce ndoa anajua kabisa kama anaenda jeshi la kujenga ukoo. Ashajiandaa kisaikolojia kabisa!, mnampa surivival 101 manual. Akikupa jikinge never hit back, jifanye umekufa kabisaa, Never talk back, akibweka kaa kimyaa. Apologise for everything hata makosa yake wewe omba msamaha, Usibishane nayee, anavyotaka ndiyo hivyoo. Jifanye mjinga hata ukiona au ukihisi vitu vipotezee tu. Aki kuprovoke jifanye zumbukuku kweli-kweli, Train Moyo wako kuweza kubeba vitu vizitoo kama insults, deception, betrayal na uwe sugu haswaa. Akirudi asubuhi unacheka cheka na chai nzitoo unaandaa. Akitaka kujieleza unamwambia haina haja nilijua umekufa kama upo hai kwangu inatosha, you out do yourself.
Kwa manual hii hata shetani unaishi nalo hata miaka 20 yaani vizuri kabisaa., Labda wewe utake kutoka sasa na kudai talaka na 50% of what you didn’t learn ukaanze sasa kusaka true love.
Na siku sasa ndiyo umeondokaa hakuna atakaye vaa viatu vyakoo. Hakuna maana hivyo viaturaizoni namba saba (7), Wiki tu ata mshindwaa na kukumbukaa zumbukuku wakee.Atakuja mapaka na wazazi wakee, atampatawapi mtu mwenye manual ya how to live with the devil?
Kuna rafiki yangu kaka wa marekani kamchukua binti wa kinondoni alafu ana manual, aah! wamehangaika kumtoa lakini wapi, nikamwambia huyo tulieni tu atatoka mwenyewe mpeni muda, ila nyie kumtoa sahauni!!!, kaka yao alizaa na mke wa kwanza mtoto mmoja 1, akasema hazai tenac, mpaka moto kafika 18, huyu udugu wetu wa kino wana miaka mitano tu na hajafunga naye ndoa wana watoto watatu tayari, ka reverse vasectomy mwenyewe, he is tameed tamed, kamuweka kiganjani kajaa. 3 Kids Marekani akija kudai child support is not a joke.